Balula :Wahitimu wa Excellent kuwa chachu kutumikia sekta ya Afya

Mgeni Rasmi katika Mhafali ya Chuo cha Afya cha Excellent  Kibaha John Mrema akizungumza katika Mahafali ya Saba ya Chuo hicho Kibaha mkoani Pwani.

Mkurugenzi wa Vyuo vya Excellent Msaada Balula akizungumza katika Mahafali ya Saba ya Chuo cha Afya cha Excellen Kibaha mkoani Pwani.

Na Mwandishi Wetu

CHUO cha Excellent Na Mwandishi Wetu Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Excellent  kimesema wahitimu wa Chuo hicho watakwenda kuwa  chachu katika kutumikia sekta ya afya   kwa weledi kutokana na mikakati  ya Chuo hicho kwa kuwa na vifaa vya afya  vya kisasa vya kufundishia pamoja na wakufunzi wabobezi.

Akizungumza katika Mahafali ya Saba ya Chuo cha Excellent Kibaha Mkurugenzi wa Vyuo vya Excellent Msaada Balula amesema kuwa wahitimu waliohitimu wana weledi wa kwenda kutumika katika sekta ya afya katika fani walizozisomea.

Balula amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa vyuo vya Excellent wahitimu zaidi 1500 ambao wameingia katika soko la ajira na kupata ujumbe kuwa wanajituma na wenye weledi katika kuhudumia jamii.

Aidha amesema kuwa wazazi wawapeleke vijana wao katila vyuo vya excellent watapata elimu na mafunzo ya kuweza kuingia katika soko la ajira kwenye sekta ya afya kutokana na kyongezeka kwa mahitaji ya watalaam yaliyochagizwa na Serikali ya awamu ya sita kujenga Hospitali ,Zahanati, pamoja vituo vya afya.

Balula aliongeza kuwa sekta ya afya lina fursa ya wataalam kujiajiri na kuendelea kutoa mchango katika taifa kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya zilizo bora.

Mgeni rasmi katika Mahafali ya Saba Chuo cha Afya cha Excellent John George amesema kuwa serikali  imewekeza katika  hospitali ,Zahanati na Vituo vya Afya ambapo uwekezaji huo unahitaji wataalam kikiwemo chuo cha Excellent.

George  amesema kuwa vyuo vya afya ikiwemo Excellent vinatoa mchango katika sekta ya afya katika kutoa huduma kwa wananchi.

Amesema Excellent imeweka mazingira ya kusomea yanayoendana na uhalisia na kufanya wanafunzi kupata utaalam unaohitajika wa kwenda kutumika sehemu za huduma za afya.

Mkuu wa Chuo cha Excellent  Kibaha Dkt.Rorgers Ndihagati amesema kuwa wahitimu  hao wameandaliwa kwa kwenda kutumikia jamii ya watanzania katika sekta ya afya.

Dkt.Ndihagati amesema kuwa Chuo kinategemea wahitimu kuwa mabalozi wa kutangaza sifa za chuo na kile wanachofanya kinaleta uhalisia wa ubalozi wao.

Rais wa Serikali ya Wanafunzi Mhitimu akitoa salamu kwa niaba ya wahitimu wenzake katika mahafali ya Saba ya Chuo cha Afya cha Excellent  Kibaha.

Mkuu wa Chuo cha Afya cha  Excellent Dkt.Rorgers Ndihagati  akizungumza katika Mahafali ya Saba ya Chuo cha Afya cha Excellen Kibaha mkoani Pwani.

Mkurugenzi wa Vyuo vya Excellent Msaada Balula akizungumza na waandishi wa habari  katika Mahafali ya Saba ya Chuo cha Afya cha Excellen Kibaha mkoani Pwani.

 Baadhi ya Wahitimu wa Chuo cha Afya cha Excellent katika Mahafali ya Saba yaliyofanyika Chuoni hapo.