Waziri Mkuu: Serikali Kuangalia Upya Migogoro Ya Ardhi Nchini

Global Publishers
March 1, 2026
0 Comments

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaangalia upya suala la changamoto ya ardhi nchini.

Amesema kuwa haiwezekani kuwepo na migogoro ya ardhi ya muda mrefu ambayo haiishi hadi kufikia hatua ya kutishia undugu miongoni mwa Watanzania.

“Inaanza kutishia Utanzania wetu, kwa hiyo hili jambo la ardhi tutaliangalia upya. Hatuwezi kuwa na jambo ambalo linakuwa sehemu ya maisha yetu. Mungu alitupa akili binadamu kuliko wanyama wengine, haiwezekani kila kona tatizo ni hilo hilo.”

Amesema hayo leo Jumapili (Machi 1, 2026) katika mkutano wa hadhara uliofanyika Stendi za Zamani, Babati Mjini mkoani Manyara.