Global Publishers
March 2, 2026
0 Comments
Kituo cha televisheni ya taifa ya Iran, Channel Two, kimethibitisha kuwa Mansoureh Khojasteh Bagherzadeh, mke wa Kiongozi Mkuu wa zamani wa Iran Ali Khamenei, ameuawa nyumbani kwake.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Bagherzadeh aliuawa katika mazingira ambayo bado hayajawekwa wazi kwa kina na mamlaka za Iran. Awali, magazeti ya ndani yalikuwa yameripoti kuwa alikuwa amepoteza fahamu, kabla ya taarifa ya televisheni ya taifa kuthibitisha kifo chake.
Vyombo vya habari vya Iran viliripoti pia kwamba katika tukio hilo, binti wa Khamenei, mjukuu wake pamoja na mkwewe walipoteza maisha.
Khamenei na marehemu mkewe walikuwa na watoto sita — wanne wa kiume na wawili wa kike. Taarifa hizi zimezua mshtuko mkubwa nchini Iran huku wananchi wakisubiri maelezo zaidi kutoka kwa vyombo rasmi vya dola kuhusu mazingira ya tukio hilo.