Mkuu wa jeshi la Uganda amesema leo Jumanne kuwa nchi yake imepeleka vikosi maalum katika mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba ili kuulinda wakati mivutano kati ya Rais Salva Kiir na Makamu wake wa Kwanza wa Rais Riek Machar ikizua hofu ya kurejea kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Hali ya wasiwasi imeongezeka katika siku za hivi karibuni nchini Sudan Kusini, mzalishaji mafuta baada ya serikali ya Kiir kuwatia ndani wawili, na maafisa waandamizi wa jeshi wanaoshirikiana na Machar.
Waziri mmoja hata hivyo ameachiliwa. Ukamataji wa Juba na mapambano yanayosababisha vifo katika mji wa kaskazini wa Nasir unaonekana kudumaza makubaliano ya amani ya mwaka 2018 yamaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka miaka, kati ya vikosi tiifu kwa Kiir na Machar vimesababisha watu 400,000 kupoteza maisha.
Katika siku mbili zilizopita, vikosi vyetu maalum vilivyoingia Juba ililinda mji, mkuu wa jeshi la Uganda, Muhoozi Kainerugaba alisema katika mfululizo wa ujumbe kwenye mtandao wa X usiku wa kuamkia Jumanne.