Global Publishers
March 18, 2026
0 Comments
Mabingwa wa Afrika, Senegal wamepokonywa rasmi taji la Africa Cup of Nations miezi miwili baada ya sherehe kubwa za ushindi, kufuatia uamuzi wa kushangaza wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Uamuzi huo umeipa Morocco ushindi wa mezani wa mabao 3-0, baada ya bodi ya rufaa ya CAF kukubaliana na malalamiko ya Morocco kuhusu tukio la fainali iliyochezwa Rabat Januari 18.
Katika dakika za mwisho za mchezo: Mwamuzi Jean Jacques Ndala alitoa penalti kwa Morocco baada ya VAR kubaini faulo ya El Hadji Malick Diouf dhidi ya Brahim Díaz
Senegal walikuwa tayari na hasira baada ya bao la Ismaïla Sarr kufutwa
Kocha wa Senegal Pape Thiaw aliwaamuru wachezaji wake kuondoka uwanjani kupinga maamuzi hayo.
Hata hivyo, Sadio Mané alijaribu kuwazuia na kuwataka warudi kuendelea na mchezo.
