Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) Wagomea Uamuzi wa CAF, Kukata Rufaa

Global Publishers
March 18, 2026
0 Comments

Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) limekosoa uamuzi wa CAF kuwatangaza kupoteza mechi ya fainali ya AFCON 2025 , na hivyo ushindi wa mabao 3–0 kutolewa kwa Morocco .

FSF limeahidi kupeleka rufaa kwa Mahakama ya Michezo (CAS) huko Lausanne. Katibu Mkuu wa FSF, Abdoulaye Sow, amesema:

“Kombe halitaondoka nchini. Senegal ina haki, na ushindi upo upande wake.”

Wachezaji pia walionyesha hisia za hasira na uchungu:

  • Idrissa Gana Gueye alisisitiza kuwa vyeo na vikombe vinaisha, lakini heshima ya mashabiki na jamii ndiyo muhimu zaidi.

  • El Hadji Malick Diouf, ambaye alihusika kwa kosa la penati, aliongeza:

“Kombe linashindaniwa uwanjani, sio kwa barua pepe.”

Bodi ya Rufaa ya CAF ilitangaza kwamba Senegal imepoteza fainali, na matokeo kuandikwa kama 3-0 kwa Morocco. Shirikisho la Soka la Morocco limekubali uamuzi, lakini limeeleza kwamba rufaa yao ilikuwa juu ya kutekeleza kanuni za mashindano pekee, si kupinga utendaji wa timu yoyote.