Simba Kupambana na Ratiba Ngumu Aprili, Macho Yote Kwa Barker

Global Publishers
March 31, 2026
0 Comments

Simba SC chini ya Kocha Mkuu Steve Barker inaingia mwezi Aprili 2026 ikiwa na ratiba ngumu ya mechi za NBC Premier League, ambapo kila mchezo ni muhimu katika harakati za kusaka alama tatu muhimu.

Baada ya mapumziko ya FIFA, “Mnyama” anarejea uwanjani na mechi saba mfululizo ambazo zinaweza kuamua mwelekeo wa msimu wake. Hizi hapa ratiba kamili:

Ratiba ya Simba SC – Aprili/Mei 2026

  • Aprili 2, 2026
    Simba SC vs Coastal Union – Saa 1:00 usiku
  • Aprili 5, 2026
    Azam FC vs Simba SC – Saa 1:00 usiku
  • Aprili 9, 2026
    Fountain Gate FC vs Simba SC – Saa 10:00 jioni
  • Aprili 15, 2026
    Namungo FC vs Simba SC – Saa 1:00 usiku
  • Aprili 19, 2026
    Simba SC vs JKT Tanzania – Saa 1:00 usiku
  • Aprili 29, 2026
    Simba SC vs Tanzania Prisons – Saa 1:00 usiku
  • Mei 3, 2026
    Simba SC vs Young Africans SC – Saa 11:00 jioni

Ratiba hii ni ngumu na yenye ushindani mkubwa, hasa mechi dhidi ya Azam FC na dabi ya jadi dhidi ya Yanga. Hizi ndizo mechi zitakazopima ubora wa kikosi cha Simba na uwezo wa kocha Barker kusimamia presha ya ubingwa.

Kipindi hiki kinahitaji umakini mkubwa, mzunguko mzuri wa kikosi, pamoja na kutumia vizuri mechi za nyumbani ili kukusanya pointi muhimu.