Admin

Mastaa Ligi Kuu wavunja rekodi CRDB Federation Cup

WACHEZAJI wanaocheza timu za Ligi Kuu Bara, wameanza vyema katika Michuano ya Kombe la Shirikisho (FA), baada ya kufunga ‘Hat-Trick’ tatu hadi sasa, ikiwa ni idadi kubwa kwa nyota hao tofauti na msimu uliopita wa 2024-2025, walipofunga moja. Msimu huu wa 2025-2026, ‘Hat-Trick’, tano zimeshafungwa ikiwa ni hatua ya 32 bora na tatu ni za…

Read More

RC Burian: Tutoe taarifa za ukatili wa kijinsia, wanawake wachangamkie mikopo ya halmashauri

Tanga. Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk Batilda Burian, ametoa wito kwa wananchi kushirikiana kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia huku akihamasisha wanawake kutumia fursa za mikopo inayotolewa na halmashauri ili kujikwamua kiuchumi. Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika leo Machi 8, 2026 katika Uwanja wa Shule ya Msingi…

Read More

Aliyechezesha Dabi ya Kariakoo apewa Kombe la Dunia 2026

Mwamuzi Amin Mohamed Amin Omar wa Misri, aliyewahi kuchezesha mechi ya ‘Kariakoo Derby’ kati ya Yanga dhidi ya Simba iliyopigwa, Juni 25, 2025, amechaguliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), kuchezesha fainali za Kombe la Dunia. Katika fainali hizo za Kombe la Dunia zitakazopigwa nchi tatu za Marekani, Canada na Mexico kuanzia Juni 11,…

Read More

Simba Queens yarudi kambini kujiandaa mzunguko wa pili WPL

SIMBA Queens imeingia kambini mapema kuanza maandalizi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Wanawake nchini, huku benchi la ufundi likieleza lengo kubwa ni kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri katika mechi zilizosalia. Kocha msaidizi wa timu hiyo, Mussa Hassan Mgosi alisema kufanya maandalizi ya mapema ni muhimu kwa kikosi hicho ili kurejea uwanjani kikiwa…

Read More

Chabruma: Mabinti msikate tamaa kupambania ndoto zenu

ALIYEWAHI kuwa kocha mkuu wa JKT Queens, Esta Chabruma amewaasa mabinti wanaocheza soka kuendelea kupambania ndoto zao bila kukata tamaa licha ya changamoto wanazokutana nazo njiani. Akizungumza na Mwanaspoti kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Chabruma alisema wanawake wengi wenye vipaji hukata tamaa mapema kutokana na vikwazo wanavyokutana navyo akasisitiza mafanikio yanahitaji uvumilivu na…

Read More

Ceasiaa yapania pointi 18 nyumbani

KOCHA wa Ceasiaa Queens, Ezekiel Chobanka amesema mipango ya timu hiyo ni kuvuna pointi 18 katika mechi sita za nyumbani zilizosalia ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kumaliza nne bora. Ceasiaa iko nafasi ya 10 kwenye msimamo wa ligi ikikusanya pointi nane kwenye mechi 11 ilizocheza, ushindi mara mbili, sare saba na kupoteza mbili. Akizungumza…

Read More

CCM yataka Kituo cha Afya Mwamapalala kianze huduma Juni

Itilima. Wakati Katibu Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kenan Kihongosi akitaka Kituo cha Afya Mwamapalala kuanza kutoa huduma Juni mwaka huu, wananchi wameeleza namna kitakavyowapunguzia adha ya kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 30 kufuata huduma za afya. Wamesema kukamilika kwake itakuwa ni mkombozi kwa wagonjwa hasa wajawazito na wazee ambao…

Read More