Admin

BALOZI DKT. NCHIMBI ATEMBELEA NYUMBANI KWA BABA WA TAIFA

Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt Emmanuel John Nchimbi ametembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, kijijini Mwitongo,Butiama na kuzuru kaburi la mwasisi huyo wa Tanzania na CCM. Dkt.Nchimbi ameingia mkoani Mara hii leo Agosti 30, 2025 akitokea mkoa wa Mwanza ikiwa ni katika harakati za…

Read More

Miradi ya Serikali Yataka Wachambuzi Wenye Maarifa Sahihi

NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV Wachambuzi wa masuala mbalimbali wamehimizwa kufanya tafiti ya kutosha kabla ya kufanya chambuzi zao ususani linapokuja suala la utekelezwaji wa miradi inayosimamiwa na Serikali ili kuepusha upotoshaji kwenye jamii  Hayo yamesemwa leo Agosti 30, 2025 Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta Binafsi na…

Read More

Ilanfya kurejea kazini baada ya kupona

MSHAMBULIAJI wa JKT Tanzania, Charles Ilanfya anarejea kazini baada ya kukaa nje ya kazi kwa muda mrefu, kutokana na kuuguza majeraha ya goti la mguu wa kulia na kusababisha kucheza mechi moja msimu uliyopita. Ilanfya aliumia Agosti 28, 2024 kwenye Uwanja wa Major Generali Isamuhyo, dakika chache baada ya kuingia kipindi cha pili mechi dhidi…

Read More

Majaliwa ataka magereza yote kutumia nishati safi kufikia 2027

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezielekeza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara ya Nishati kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha magereza yote nchini yanaunganishwa na mfumo wa nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2027. Majaliwa amesema hatua hiyo inalenga kuboresha mazingira ya wafungwa, kulinda afya za watumishi na kuunga mkono jitihada za Serikali katika…

Read More

Mahakama yaipa nafuu Chadema | Mwananchi

Arusha. Mahakama Kuu Kanda ya Manyara, imekubali maombi ya Bodi ya Wadhamini wa Chadema ya kufungua shauri la maombi ya mapitio kupinga uamuzi wa Msajili wa Vyama vya Siasa, aliyetengua uteuzi wa viongozi wa sekretarieti ya chama hicho. Vilevile, imesimamisha uamuzi wa msajili huyo wa Mei 27, 2025 uliozuia Chadema kuendelea kupokea ruzuku, kusubiri uamuzi…

Read More

Miradi ya Sh164 bilioni kutembelewa na mbio za mwenge

Geita. Miradi 61 yenye thamani ya zaidi ya Sh164 bilioni inatarajiwa kutembelewa, kukaguliwa, kuwekewa mawe ya msingi na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka huu mkoani Geita, ikiwa ni ongezeko la zaidi ya asilimia 500 ya thamani ya miradi iliyotembelewa mwaka 2024. Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigela ameyasema hayo leo Septemba 30, 2025,…

Read More

Geay ajenga kambi ya kisasa ya riadha

MWANARIADHA wa kimataifa wa Tanzania, Gabriel Geay, ameandika ukurasa mpya katika riadha nchini kwa kujenga kambi ya kisasa kwenye kijiji cha Madunga wilayani Babati, Mkoa wa Manyara. Lengo la kambi hiyo ni kuibua na kuendeleza vipaji vya vijana wa Kitanzania na kuandaa mashujaa wa kesho watakaoiwakilisha nchi katika mashindano makubwa ikiwemo michezo ya Olimpiki. Kambi…

Read More

Takukuru yabaini madudu miradi ya Sh6.6 bilioni

Moshi. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Kilimanjaro, imebaini mapungufu katika miradi 11 ya maendeleo yenye thamani ya Sh6.68 bilioni mkoani Kilimanjaro. Akitoa taarifa ya utekelezaji katika kipindi cha Aprili hadi Juni 2025, Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kilimanjaro, Musa Chaulo, amesema katika kipindi hicho taasisi hiyo ilifuatilia utekelezaji wa miradi…

Read More

ACT-Wazalendo, Monalisa wavutana | Mwananchi

Dar es Salaam. Wakati uongozi wa tawi la ACT-Wazalendo la Mafifi mkoani Iringa, ukitangaza kumfuta uanachama kada wake Monalisa Ndala, yeye ameibuka akipinga hatua hiyo. Monalisa amepinga hatua hiyo akibainisha kuwa yeye bado ni mwanachama hai wa ACT-Wazalendo tawi la Kibangu, wilayani Ubungo, mkoani Dar es Salaam na siyo Mafifi kama ilivyoainishwa katika barua ya…

Read More