Admin

TANESCO YAKAMATA WATU WATANO WAKIHUJUMU UMEME KAHAMA

Afisa Usalama wa TANESCO Mkoa wa Tabora na Msimamizi wa Usalama wa Kanda ya Magharibi, Said Sombwe, akionesha eneo ambalo wizi wa umeme ulikuwa ukifanyika wakati wa oparesheni maalum ya BAOMA wilayani Kahama. Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewakamata watu watano katika Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, kwa…

Read More

Samia: Morogoro ya viwanda inarudi

Morogoro/Mwanza. Chama cha Mapinduzi (CCM), kimeendelea na kampeni kikiahidi kuirejeshea Morogoro hadhi yake ya kuwa mkoa wa viwanda, huku ikieleza itakachowafanyia wananchi wa Mwanza.   Mgombea urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan, leo Agosti 29, 2025 akiwa mkoani Morogoro ameahidi kuurejesha katika hadhi yake kama mkoa wa viwanda ili kuibua fursa nyingi za ajira kwa…

Read More

Hekaheka wiki ya kwanza kuzisaka kura urais 2025/30

Dar es Salaam. Hekaheka za kusaka kura za nafasi ya urais katika wiki ya kwanza ya kampeni tayari zimeanza na kuvifanya vyama vya siasa kugawana maeneo ya nchi, kunadi sera zao kushawishi wananchi, ili wagombea wao wachaguliwe. Chama cha Mapinduzi (CCM) ndicho kilichofungua pazia la kumnadi mgombea wake, Samia Suluhu Hassan, sambamba na mgombea mwenza…

Read More

Msipeleke watoto vilabuni, Jeshi la Polisi laonya

Iringa. Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa limewaonya wazazi na walezi kuacha tabia ya kuwapeleka watoto kwenye vilabu vya usiku, likieleza kuwa maeneo hayo yanachochea mmomonyoko wa maadili na kuwaweka watoto katika hatari ya ukatili wa kijinsia na kiafya. Onyo hilo limetolewa Agosti 28, 2025 na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa…

Read More

Tanzania kudhibiti kemikali hatari za dawa za kulevya

Nashville. Tanzania imeingia makubaliano na nchi zinazozalisha kwa wingi kemikali bashirifu zinazotumika katika utengenezaji wa dawa za kulevya ili kupunguza athari kwa vijana. Hayo yamesemwa na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo ambaye ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki Mkutano wa 39 wa Kimataifa wa Mapambano Dhidi…

Read More

Tanzania ijifunze haya, mdororo wa uchumi Botswana

Kupungua kwa mauzo ya almasi kumetajwa kama moja ya sababu iliyofanya nchi ya Botswana kutangaza hali ya dharura kutokana na kushindwa kumudu baadhi ya mahitaji ikiwamo katika sekta ya afya. Agosti 26, 2025 Botswana ilitangaza hali ya dharura ya afya ya umma kutokana na kukabiliwa kwa uhaba wa dawa muhimu na vifaa vya matibabu. Rais…

Read More

TLP yaahidi kampeni za amani, utulivu

Dar es Salaam. Chama cha Tanzania Labour Party (TLP), kinatarajia kuzindua kampeni zake Septemba 4, 2025 huku kikiahidi kuwa zitafanyika kwa amani na utulivu. Hayo yameelezwa leo Ijumaa Agosti 29, 2025 na mgombea urais wa chama hicho, Yustas Rwamugira, katika hafla ya wananchama kumpokea iliyofanyika makao makuu ya chama hicho Magomeni, Dar es Salaam akitokea…

Read More

Mastaa Simba watambia usajili | Mwanaspoti

WAKATI Simba ikirejea nchini alfajiri ya leo ikitokea Misri, mastaa wa timu hiyo wameringia usajili wa kikosi hicho kwa msimu msimu mpya wakisisitiza wamepania kufanya mabadiliko. Simba iliweka kambi jiji la Ismailia kabla ya kuhamia Cairo, Misri ikitumia siku 31 kujifua tayari kwa msimu wa 2025/26 ambao utaanza rasmi Septemba 16 kwa kupigwa mechi ya…

Read More