Admin

Fountain Gate yalamba dili | Mwanaspoti

TIMU ya Fountain Gate imeingia makubaliano ya miaka miwili yenye lengo la kuhakikisha kwamba wachezaji na benchi la ufundi wanakuwa katika mazingira bora ya kiutendaji wanapokuwa katika majukumu yao uwanjani. Dili jipya la timu hiyo ukiondoa yale ya udhamini wa jumla katika Ligi Kuu Bara yanayotolewa na wadhamini wa michuano hiyo, limetoka katika maji ya…

Read More

Bunge lawaita wananchi kushiriki marathoni

MBUNGE wa Makete na Mwenyekiti wa Bunge Bonanza, Festo Sanga amewataka wananchi kujumuika na wabunge katika mbio za marathoni za Bunge zinazotarajiwa kufanyika Julai 18, mwaka huu. Mbio hizo zinalenga kuchangia damu salama na kuimarisha afya. Marathoni hiyo ambayo ni ya msimu wa tatu inatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Jamhuri, Dodoma ikikutanisha wakimbiaji wa kilomita…

Read More

Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Suleiman Abdulla awaongoza wateja, wadau wa NBC kushiriki hafla ya futari Zanzibar

Pamoja na ushiriki huo Mhe Abdulla aliishukuru na kuipongeza NBC kwa kuandaa tukio hilo la kiimani, akieleza kuwa ni ishara ya moyo wa kujali na kujenga mahusiano imara na jamii. Alitoa shukrani za dhati kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kutambua mchango wa NBC katika maendeleo ya visiwa hivyo—kuanzia msaada wa kifedha, ushauri…

Read More

NDUNA MKOMANILE ANG’ARA RUVUMA: WANANCHI WAJIFUNZA MCHANGO WA WANAWAKE KATIKA VITA VYA MAJIMAJI

Wananchi mbalimbali pamoja na baadhi ya viongozi wamepata fursa ya kutembelea onyesho maalum la Nduna Mkomanile lililofanyika katika Kituo cha Baraza la Wazee wa Mila na Desturi Mkoa wa Ruvuma. Onyesho hilo limefanyika tarehe 27/02/2026, likiwakutanisha wadau mbalimbali waliotaka kujifunza na kutambua mchango wa wanawake katika historia ya ukombozi wa taifa. Nduna Mkomanile anatambulika kama…

Read More

Wakulima wa parachichi walilia ukaguzi wa mizani

Rungwe. Wakulima wa Parachichi Wilaya ya Rungwe, mkoani Mbeya wameomba Wakala wa Vipimo (WMA), mkoani hapa kuingilia kati na kufanya ukaguzi wa kushtukiza ili kubaini uchakachuzi wa mizani ya kidigitali kutumika kuwaibia. Hatua hiyo imekuja kufuatia malalamiko ya muda mrefu ya wakulima hususani maeneo ya vijijiji kudai wanunuzi kutumia mizani iliyo nembo za mamlaka husika…

Read More

Offen Chikola ni mapambano tu

KIUNGO mshambuliaji wa Singida Black Stars, Offen Chikola amesema msimu huu upande wake ni wa kujifunza vitu vingi, huku akiwa amecheza kwa dakika 50 pekee dhidi ya Fountain Gate tangu ajiunge na timu hiyo kwa mkopo kipindi cha dirisha dogo Januari 2026 akitokea Yanga. Chikola aliyejiunga na Yanga msimu huu kwa mkataba wa miaka mitatu…

Read More

Mtanzania adai kuteswa Uarabuni, aomba msaada kurejeshwa Tanzania

Dar es Salaam. Wakati Afrika Mashariki ikiendelea kufuatilia kwa hofu hatima ya mfanyakazi wa ndani kutoka Uganda, Vicky Ajok, anayekabiliwa na hukumu ya kunyongwa nchini Syria, simulizi nyingine ya maumivu inamhusu Mtanzania, Zaidatu Hasani Rashid, anayepitia mateso katika Falme za Kiarabu na sasa anataka kurudi Tanzania. Zaidatu alisafiri Agosti 30, 2025 kwenda katika nchi hiyo…

Read More