Admin

Malale akaribishwa KVZ kwa kichapo

TIMU ya KVZ inayofundishwa na Malale Hamsini, imepokea kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa bingwa mtetezi wa Ligi Kuu Zanzibar, Mlandege, katika mechi ya ligi hiyo iliyochezwa jana Desemba 16, 2025 kwenye Uwanja wa Mao A, uliopo Mjini Unguja. Bao lililofungwa na Yussuf Suleiman dakika ya sita, ndilo lililoishusha KVZ kutoka nafasi ya pili hadi…

Read More

FYATU MFYATUZI: Tulaani mabeberu mabarubaru na maburebure! Ndivyo ilivyo

Kuna mafyatu wanatubagaza na kutushangaza. Si mabeberu ‘wameleta’ vuguvugu na vurugu kayani! ‘Wamehonga’ watoi na mafyatu wakiwashe na kukinukisha kiasi cha wote kunuka wakahujumu amani ya imani kupitia ‘vurugu’ eti ya kudai haki. Wamewadanganya kuwashinikiza mdai haki mkaponzwa. Eti hamna haki! Haki gani katika kaya ya amani yenye ajira lukuki? Nani asiyepata haki hadi akataka…

Read More

NIKWAMBIE MAMA: Mzalendo ni gaidi wa kaburu

Siku moja Mwalimu Nyerere alisema kuwa aliona wakubwa wakienda kufanya azimio Zanzibar. Alipowaona wakirudi kimya kimya na sera za uchumi zikibadilika kufuata matakwa ya WB na IMF, akawa na uhakika kuwa ndoto zake za Azimio la Arusha zilikuwa zimefikia ukingoni. Mwenyewe alijua fika kuwa Azimio la Arusha lilikuwa ni chukizo kubwa kwa wakoloni na wanyonyaji….

Read More

KONA YA MALOTO: Naomba kuchangia hekima kidogo na Padri Kitima

Hekima ya wana wa dunia waliotangulia kuuishi ulimwengu, walisema: “Ukivuliwa nguo chutama.” Oktoba 29, 2025, Tanzania ilivuliwa nguo. Jitihada zote za kujisahihisha zinabeba tafsiri ya kuchutama. Hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan, wakati wa uzinduzi wa Bunge la 13, Bungeni, Dodoma, Novemba 14, 2025, alikiri nchi kuvuliwa nguo. Aliomba nafasi ya kujirekebisha. Aliahidi maridhiano. Mambo…

Read More

Wanapokosea upinzani kusaka dola nchi za Afrika

Dar es Salaam. Safari ya vyama vya upinzani barani Afrika katika kuisaka dola inaendelea kuwa ngumu na yenye miiba, huku vikwazo vya kisiasa, kisheria na kiusalama vikizidi kutishia uhai na mustakabali wa viongozi wake. Licha ya kuanzishwa kwa vyama vya upinzani kwa dhamira ya kuimarisha demokrasia, kutoa mbadala wa sera na kuikosoa serikali kwa uwajibikaji,…

Read More

Aliyekiri kuua kwa kudai kuvuta bangi, ahukumiwa kunyongwa

Arusha. Bingwa wa kupangua adhabu ya kifo anasa, ndivyo unaweza kuelezea namna Kinyota Kabwe aliyepangua adhabu ya kifo mara mbili, alivyotiwa hatiani tena na kuhukumiwa kifo kwa mara ya tatu kwa kosa lilelile alilolitenda miaka 12 iliyopita. Mara ya kwanza alihukumiwa adhabu ya kifo mwaka 2017 lakini akakata rufaa na mahakama ikaamuru kesi isililizwe upya,…

Read More