Serikali kushughulikia waajiri wanaozuia watumishi kujiunga vyama vya wafanyakazi
Arusha. Serikali imesema itaanza kuwachukulia hatua za kisheria na kinidhamu waajiri wote nchini watakaowazuia wafanyakazi wao kujiunga na vyama vya wafanyakazi. Hayo yamesemwa leo Septemba 15, 2025 jijini Arusha na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu Zuhura Yunus wakati akifungua semina ya siku tano kwa waajiri na viongozi…