Marekebisho sheria ya ndoa bado mfupa mgumu, Serikali yataja mikakati kuinasua
Dodoma. Wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu wakipaza sauti zao kutaka sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ifanyiwe marekebisho ili kumpa nafasi mtoto wa kike kupata elimu, Serikali imesema kuwa inafanya jitihada mbalimbali za kukamilisha mchakato huo. Sheria hiyo ya ndoa imeruhusu mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 14 kuolewa kwa idhini ya…