JICHO LA MWEWE: Fei Toto na Yanga wapendane ili iweje!
NDIO mpira wenyewe ulivyo. Namaanisha namna ambavyo Yanga wanachukiana na Fei Toto, au tuseme ambavyo Fei Toto anavyochukiana na Yanga. Ndio mpira wenyewe. Wapendane ili iweje? Kwani waliachanaje? Nilimsikia shabiki mmoja wa Yanga, Ray Kigosi akilalamika namna ambavyo Fei aliweka kidole mdomoni kama ishara ya kuwanyamazisha mashabiki wa Yanga baada ya kufunga penalti yake wiki…