Taifa Stars ipo tayari kuivaa Zambia
TAIFA Stars jana ilijifua kwa mara ya mwisho katika kujiandaa na mchezo wa tatu wa kuwania kufuzu ushiriki wa fainali za Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Zambia utakaopigwa Jumanne, huku mastaa karibu wote wakionyesha wanaitaka mechi hiyo itakayopigwa ugenini. Jana asubuhi kikosi hicho chini ya makocha Hemed Suleiman ‘Morocco’ na Juma Mgunda kilipiga tizi…