Admin

Airtel Tanzania yazindua Maduka 17 ya Smart Shops Dar es Salaam, kukuza Huduma za Kidijitali

 Airtel Tanzania, kampuni inayoongoza huduma za mawasiliano nchini, imezindua maduka mapya 17 ya Airtel Smart Shops jijini Dar es Salaam. Maduka haya ni sehemu ya mtandao wa maduka 31 nchini kote, ukiwa na lengo la kupanua huduma za kidijitali na kuongeza ujumuishaji wa kifedha kwa wananchi. Uzinduzi huo uliofanyika Machi 12, 2026, ulihudhuriwa na Mhe. Angellah…

Read More

Bilioni 388.8 kujenga Afcon City Unguja

WAKATI Tanzania ikiwa miongoni mwa nchi zitakazokuwa wenyeji wa Fainali za Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) 2027, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema imejiandaa vizuri kupokea ugeni huo kwa kuanzisha mradi wa michezo uliopewa jina la Afcon City. Mradi huo unaojengwa Fumba kisiwani Unguja, unatarajiwa kugharimu dola za Marekani milioni 150 (Sh388.8 bilioni za…

Read More

Chamou aendeleza rekodi dhidi ya Namungo

BEKI wa kati wa TRA United, Chamou Karaboue, ameendeleza rekodi bora katika Ligi Kuu Bara msimu huu, baada ya nyota huyo kufikisha mabao mawili, ambayo yote ameyafunga dhidi ya ‘Wauaji wa Kusini’, Namungo, huku akichezea timu mbili tofauti. Nyota huyo anayeichezea TRA United kwa mkopo akitokea Simba, alianza kufunga akiwa na kikosi hicho cha Msimbazi,…

Read More

Dalali wa Mahakama akamatwa, agizo la Dk Mwigulu halijatekelezwa

Arusha. Zikiwa zimepita siku 17 tangu agizo la Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba la kurejeshwa mali za mfanyabiashara wa Arusha, Josephine Shirima, mali hizo bado hazijarudishwa huku Jeshi la Polisi likimshikilia dalali wa Mahakama anayedaiwa kuhusika katika kuchukuliwa kwa mali hizo. Aidha, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Wilaya ya Arusha, Dominic Mollel, aliyekuwa anashikiliwa na polisi kwa…

Read More

Singida alenga ushindi dhidi Mbeya City

BAADA ya kudondosha pointi sita katika mechi mbili Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga na Simba, kocha wa Singida Black Stars, David Ouma amewataka wachezaji wake kusahau matokeo hayo na kuelekeza nguvu katika mchezo dhidi ya Mbeya City. Ouma alisema licha ya kupoteza michezo hiyo migumu anaamini kikosi chake kilionyesha kiwango kizuri na kilistahili kupata…

Read More

TANZANIA YAJINADI UIMARISHAJI USAWA WA KIJINSIA NA UPATIKANAJI WA HAKI KWA WANAWAKE MKUTANO WA CSW 70.

Na WMJJWM New York Marekani Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesisitiza mshikamano wake na nchi wanachama wa jumuiya ya kimataifa katika kuendeleza ajenda ya usawa wa kijinsia duniani. Akizungumza katika mkutano wa 70 wa kimataifa kuhusu masuala ya wanawake na haki, mwakilishi wa Tanzania katika Mkutano huo Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia,…

Read More

Mahakama Kuu Yaamuru Kufungwa kwa Sahara Media Group Limited

Mahakama Kuu Kitengo cha Biashara imeamuru kufungwa kwa kampuni ya Sahara Media Group Limited, iliyojishughulisha na vyombo vya habari, matangazo na huduma za uchapishaji, kutokana na hali mbaya ya kifedha. Uamuzi huo umetolewa na Jaji Dk. Mwajuma Kadilu baada ya kuridhia ombi la kufilisi lililowasilishwa na kampuni yenyewe. Ombi hilo liliungwa mkono na kiapo cha…

Read More