Mwenyekiti wa kijiji mbaroni kwa madai ya kumpa ujauzito mwanafunzi
Moshi. Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamshikilia Mwenyekiti wa Kijiji cha Mlangoni, Wilaya ya Siha mkoani humo, Ezekiel Mloli kwa madai ya kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha nne katika moja ya shule za sekondari wilayani humo. Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk Christopher Timbuka amethibitisha kutokea kwa tukio hilo akidai mtuhumiwa huyo anashikiliwa kwa…