Mahakama yabatilisha hukumu ya kifungo miaka 20 kwa raia wa kigeni
Arusha. Mahakama ya Rufani imebatilisha hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela aliyokuwa amehukumiwa raia wa kigeni, Lonie Rayford na kuamuru aachiwe huru baada ya kubaini kuwa hapakuwepo ridhaa ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), ya kusikilizwa kwa kesi yake. Raia huyo alidaiwa Julai 4, 2018 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere…