Mbinu mpya uingizaji wa mihadarati zinatia hofu
Biashara haramu ya dawa za kulevya inaendelea kubadilika kadiri mamlaka zinavyoimarisha udhibiti wake. Hivi sasa, wafanyabiashara wa dawa hizo wamebuni mbinu mpya ya kuziingiza Zanzibar, hali inayoongeza wasiwasi kuhusu usalama wa jamii, hususan watoto na vijana. Mbinu hii mpya imeibuka baada ya njia nyingi zilizokuwa zikitumiwa kwa muda mrefu, zikiwemo kuzimeza na kuzibeba tumboni, kugundulika…