MWANDISHI NGURI AMSHAURI RAIS SAMIA JINSI YA KULIPONYA TAIFA
………………. Na Jackton Manyerere Kwa miaka mingi, Tanzania imekuwa kisiwa cha amani katika bahari yenye misukosuko ya migogoro barani Afrika. Tulijenga taifa letu juu ya misingi ya haki, utu, na umoja. Hizi ni tunu ambazo Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliziita nguzo za uhai wa taifa. Lakini leo, nchi yetu iko katika kipindi kigumu cha majaribu…