BANDA LA DAWASA LAWAVUTIA WENGI SIKU YA WAHANDISI
Wananchi mbalimbali wamejitokeza kwenye banda la maonyesho la Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) katika maadhimisho ya siku ya Wahandisi Kitaifa yanayoendelea ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Katika Banda la DAWASA wadau wanaojitokeza kupata fursa ya kupata elimu mbalimbali za Mamlaka ikiwemo elimu ya huduma za maji,…