Sumaye asema Samia amedumisha amani, utulivu nchini

Mwanga/Same. Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania, Frederick Sumaye amesema miaka minne ya utawala wa Samia Suluhu Hassan umedhihirisha uimara wake wa kudumisha amani na utulivu nchini na kurudisha uhusiano wa kidiplomasia duniani. Wakati Sumaye akieleza hayo, mgombea mwenza wa urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amesema Samia anaishi kiapo alichokiapa cha kuilinda…

Read More

ATTF na Arthshakti Foundation Kushirikiana Kutoa Elimu ya Matumizi Sahihi ya Mitandao na Kuendeleza Uchumi Jumuishi

Na Karama Kenyunko, Michuzi Tv Taasisi ya Africa’s Think Tank Foundation (ATTF) kwa kushirikiana na Arthshakti Foundation nchini Tanzania imesema itaendelea kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025. Kwa mujibu wa taasisi hizo, kumekuwapo na ongezeko la matumizi mabaya ya…

Read More

JAMBO GROUP MDHAMINI MKUU PAMBA JIJI FC

Viongozi wa Jambo Group na viiongozi wa Pamba Jiji FC katika picha ya pamoja.Pamba jiji FC wakitembelea kiwanda cha Jambo Food product. Na Eunice Kanumba-Shinyanga Kampuni ya Jambo Group ya mjini Shinyanga sasa ni mdhamini mkuu wa timu ya Pamba FC ya jijini Mwanza katika msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuanza rasmi Septemba…

Read More

Shigela: Wananchi heshimuni sheria bila shuruti

Geita. Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigela amewataka wananchi kuheshimu vyombo vya dola na kutii maelekezo yake bila shuruti hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.Akizungumza leo Septemba 14,2025,wakati wa kukabidhi magari mapya 15 kwa jeshi la polisi mkoani humo, Shigela amesema ni desturi ya Watanzania kuheshimu askari polisi, hivyo ni vyema kuendeleza…

Read More

Mngulumi na Deus waungana kusaka kura za CCM Kongwa

Kongwa. Mgombea ubunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kongwa, Isaya Mngulumi anafanya kazi na waliokuwa wagombea wenzake ili kutafuta kura. Kitendo hicho kinatajwa kuwa mkakati wa kumaliza makundi ndani ya chama. Hata hivyo, aliyeshika nafasi ya tatu katika kura za awali Deus Seif ameonekana kuwa turufu ya chama hicho ndani ya jimbo akitakiwa…

Read More

Dk Tulia aahidi kuanza na vipaumbele 15 Jimbo la Uyole

Mbeya. Mgombea ubunge wa Jimbo jipya la Uyole kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Tulia Ackson, ametaja vipaumbele 15 ambavyo amesema vitabadili taswira ya Uyole ifikapo mwaka 2030, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa halmashauri mpya itakayojitegemea kimapato. Ametoa kauli hiyo jana Jumamosi, Septemba 13, 2025, katika uzinduzi wa kampeni uliofanyika Shule ya Msingi Hasanga,…

Read More

Tanzania na Algeria kushirikiana katika upatikanaji wa dawa salama, bora na fanisi.

Tanzania na Algeria zimekubaliana kushirikiana katika kuboresha uhusiano kwenye upatikanaji na uzalishaji wa dawa zenye usalama, ubora na ufanisi  katika nchi hizo. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Dawa nchini Algeria  alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Wizara ya Afya Tanzania uluoongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkr. Adam Fimbo pamoja na Balozi wa Tanzania…

Read More

Wananchi wa Kalila walia zahanati kutokamilika

Rukwa. Wananchi wa Kijiji cha Kalila, Kata ya Kabwe, Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa, wameiomba Serikali kukamilisha ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho, ambayo imeshindwa kukamilika kwa muda mrefu sasa. Wamesema kutokana na kadhia hiyo, wajawazito hujikuta wakijifungulia njiani au majini wakiwa kwenye mitumbwi wakifuatilia huduma hiyo katika maeneo mengine. Wakizungumza na Mwananchi leo Jumapili,…

Read More