Wastani wanawake wanne hukatwa matiti kila wiki KCMC

Moshi. Wakati takwimu zikionesha kuwa asilimia 14.4 ya wanawake nchini wanaugua saratani ya matiti, Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC, imesema baadhi yao hufika wakiwa katika hatua ya tatu na nne ya ugonjwa hali ambayo inapelekea wastani wa  wanawake wanne kukatwa matiti kila wiki. Hayo yamesemwa leo Jumapili Machi 8. 2026 na Ofisa…

Read More

RC Burian: Tutoe taarifa za ukatili wa kijinsia, wanawake wachangamkie mikopo ya halmashauri

Tanga. Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk Batilda Burian, ametoa wito kwa wananchi kushirikiana kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia huku akihamasisha wanawake kutumia fursa za mikopo inayotolewa na halmashauri ili kujikwamua kiuchumi. Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika leo Machi 8, 2026 katika Uwanja wa Shule ya Msingi…

Read More

CCM yataka Kituo cha Afya Mwamapalala kianze huduma Juni

Itilima. Wakati Katibu Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kenan Kihongosi akitaka Kituo cha Afya Mwamapalala kuanza kutoa huduma Juni mwaka huu, wananchi wameeleza namna kitakavyowapunguzia adha ya kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 30 kufuata huduma za afya. Wamesema kukamilika kwake itakuwa ni mkombozi kwa wagonjwa hasa wajawazito na wazee ambao…

Read More

Wanawake FCC watakiwa kujenga Mshikamano na Umoja

Na Mwandishi Wetu Wanawake wa Tume ya Ushindani (FCC ) wametakiwa kuwa na  upendo ambao utajenga mshikamano na kuleta ufanisi katika Taasisi. Hayo ameyasema Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Magdarena Utouh katika  Maadhimisho  ya Siku ya  Wanawake Duniani ambayo hufanyika kila Machi 8 ya kila mwaka. Magdelena amesema maadhimisho ya Siku ya…

Read More

Mbunge aeleza chanzo cha ajali yake msafara wa PM

Moshi. Mbunge wa Moshi Mjini (CCM), Ibrahim Shayo amesema ajali aliyopata Februari 18, 2026 haikuhusisha mkono wa mtu kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakidai. Shayo amesema chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka kwa tairi la mbele la gari walilokuwa wakisafiria, hali iliyosababisha dereva kushindwa kulimudu kutokana na gari hilo kuwa katika mwendo mkali. Ameyasema…

Read More