Joto kazini laua 18,970 kila mwaka duniani

Arusha. Wafanyakazi zaidi ya milioni 22 duniani wanapata madhara ya ajali sehemu za kazi, huku wengine 18,970 wakifariki duniani kote kila mwaka kutokana na ongezeko la joto mahali pa kazi. Mbali na waajiri kuweka mazingira rafiki sehemu ya kazi, waajiriwa wametakiwa kutambua kwamba wana wajibu wa kuhakikisha wanasimamia usalama wao pindi wawapo kazini. Hayo yamebainishwa…

Read More

SERIKALI YATOA BIL 1.5 UREJESHAJI MIUNDOMBINU YA BARABARA MWANZA

Serikali imetoa shilingi Bilioni 1.5 kwa ajili ya kuanza urejeshaji wa miundombinu ya barabara zilizoharibika maeneo mbalimbali Mkoani Mwanza. Fedha hizo zimetolewa na serikali kwenda Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Mwanza ili kuanza haraka kazi ya marekebisho miundombinu ya barabara na madaraja ambayo yameharibika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Meneja wa TANROADS Mkoa…

Read More

Wahariri kujadili mabadiliko ya tabianchi

Dodoma. Wahariri nchini wanakutana jijini Dodoma kujadili masuala yanayohusu nchi na ustawi wa vyombo vya habari, mada kuu ikiwa nafasi ya vyombo hivyo katika matumizi ya gesi asilia kwa ajili ya kulinda misitu. Hayo yameelezwa leo Jumapili Aprili 28, 2024 na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Neville Meena alipozungumza…

Read More

RAIS AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndugu Winfrida Beatrice Korosso kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndugu Bibiana Joseph Kileo kuwa Naibu…

Read More

Wafugaji wataka bima ya mifugo

Dar es Salaam. Wafugaji wameomba kuwe na bima ya mifugo iwapo watakufa au kupata ajali, ambayo itafungua fursa zaidi za soko la ajira katika mnyororo wa thamani. Akizungumza leo Jumapili Aprili 28, 2024 katika hafla ya Siku ya Uwekezaji ya Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Wafugaji Tanzania, Mrida Marocha amesema wanahitaji bima ya mifugo ambayo…

Read More

Chongolo acharuka, ataka uchunguzi ujenzi wa bweni

Songwe. Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani humo,  kufanya uchunguzi wa matumizi ya fedha kwenye ujenzi wa bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule ya msingi Ipapa iliyopo wilaya ya Ileje kwa gharama ya zaidi ya Sh100 milioni. Chongolo ametoa agizo…

Read More

Miili miwili ya walioangukiwa na ukuta yazikwa Dar

Dar es Salaam. Miili ya watu wawili kati ya wanne wa familia moja waliofariki dunia kwa kuangukiwa na ukuta wa nyumba waliyokuwa wakiishi imezikwa. Ajali hiyo ilitokea Mtaa wa Goroka B, Toangoma, mkoani Dar es Salaam. Miili mingine imesafirishwa kwenda mkoani Kigoma. Ajali ilitokea asubuhi ya Aprili 26, 2024. Waliofariki dunia ni Lidya Heza (21),…

Read More

Jiji la Dodoma hatarini kuwa eneo la makazi holela

Dodoma. Tangu Dodoma ilipotangazwa kuwa Jiji Aprili 2018, kumekuwa na kasi kubwa ya ongezeko la idadi ya watu na shughuli za kibinadamu zinazoathiri mifumo ya ikolojia hasa misitu na uoto wa asili. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi, idadi ya watu jijini humo imeongezeka kutoka 410,956 mwaka 2012 hadi 765,179 mwaka 2022 sawa…

Read More

Simulizi ya mwanafunzi mchoraji mwenye uoni hafifu

Bukoba. “Nilianza kuchora picha ya chupa ya maji, baadaye nilichora picha ya baba yangu mzazi, kwa sasa nimechora picha ya mbunge wangu, na picha hii ni zawadi kwake. Natamani kusoma chuo  Korea na China ili kuendeleza kipaji changu na kuinua familia yangu yenye uhitaji mkubwa.” Hayo ni maneno ya Julieth Richard (19), msichana mwenye uoni…

Read More