Boeing 737-9 Max kuanza kutua Dodoma

Dodoma. Wakati Bunge la Tanzania likipitisha bajeti ya Wizara ya Uchukuzi, Serikali imesema mwishoni mwa mwaka 2024 ndege kubwa ya abiria ya Boeing 737-9 Max itaanza kwenda Dodoma mara mbili kwa siku. Pia, Serikali imesema wananchi wa Kipunguni jijini Dar es Salaam waliopisha uwanja wa ndege, wataanza kulipwa fedha zao mwaka huu, baada ya kusubiri…

Read More

Mashekhe Arusha Wakoshwa na Ujio wa Makonda Arusha.

Na Jane Edward, Arusha Sheikh Hussein Said Junje, Sheikh wa Wilaya ya Arusha Mjini amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Mhe. Paul Christian Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha akimsifu kwa Uwajibikaji wake katika kusimamia haki za wananchi wa Arusha. Sheikh Junje ametoa kauli hiyo Ofisini…

Read More

RAIS SAMIA AAGIZA HUDUMA ZA DHARURA MAENEO YALIYOATHIRIWA NA KIMBUNGA HIDAYA

RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan ameagiza huduma za dharura zipelekwe kwenye maeneo yaliyopata athari kutokana na kimbunga Hidaya. Hayo yamesemwa leo (Mei 6, 2024) na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwenye kikao cha dharura cha Kamati ya Maafa Kitaifa alichokiitisha kupokea taarifa ya hatua zilizochukuliwa kwenye maeneo yaliyopata athari. “Rais ameelekeza hatua za haraka zichukuliwe katika…

Read More

Majaliwa ataka wateule wa Rais kusimamia haki

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  amewataka wakuu wa mikoa kuyasimamia na kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa na Tume ya Haki Jinai. Aidha,  amesisitiza kwamba ni lazima viongozi na watendaji wa Serikali wawe na uelewa wa kutosha ili waweze kuyasimamia na kuyatekeleza mapendekezo hayo. Waziri Mkuu amebainisha hayo leo Mei 6, 2024 wakati akifungua warsha ya…

Read More

BASHUNGWA APIGA KAMBI LINDI, KUHAKIKISHA BARABARA YA DAR – LINDI INAPITIKA NDANI YA SAA 72.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amewatoa hofu na kuwahakikishia wananchi, wasafiri na wasafirishaji kuwa ameweka kambi Mkoa wa Lindi kuhakikisha anasimamia timu ya watalaamu wa Wakala ya Barabara (TANROADS) na makandarasi, kuhakikisha wanakamilisha kazi ya kurejesha mawasiliano ya barabara ya Lindi – Dar es Salaam ndani ya saa 72. Waziri Bashungwa ameeleza hayo, leo tarehe…

Read More

Ma- DED wanolewa kuhusu uchaguzi, rushwa na mikopo

Kibaha. Wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa nchini kote leo Mei 6, 2024, wameanza mafunzo ya siku tatu yenye lengo la kuwaongezea mbinu za kuboresha utekelezaji wa majukumu yao mahala pa kazi. Mada zitakazotolewa wakati wa mafunzo hayo yanayofanyika Kibaha mkoani Pwani ni pamoja na masuala ya rushwa na ubadhirifu katika mamlaka za Serikali…

Read More