Watanzania watakiwa kuzingatia ubora wa bidhaa

Dar es Salaam. Watanzania wametakiwa kuzingatia ubora wanaponunua bidhaa, ili kuepuka hasara kwa kununua bidhaa zisizodumu na zinazotumia nishati nyingi.  Hayo yameelezwa jana Aprili 19, 2024 katika mkutano wa uzinduzi wa bidhaa za viyoyozi (AC) zinazouzwa na kampuni ya Haier Tanzania. Kampuni ya Haier iliingia rasmi ubia na kampuni ya GSM Group mwaka 2023 kwa…

Read More

NCCR yasema uchumi wake hauruhusu kufanya mikutano

Dar es Salaam. Viongozi wa Chama cha NCCR Mageuzi wametakiwa kurudi majimboni mwao ili kuwahamasisha wananchi kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa na kukijenga chama. Hatua ya chama hicho imekuja baada ya kile kinachoelezwa hali ya uchumi wa chama hicho kutowaruhusu kufanya  mikutano ya hadhara kama vyama vingine. Kuwaambia viongozi wao warudi majimboni ni moja…

Read More

Waziri Mkuu kuongoza majaribio SGR Dar-Dodoma Aprili 21

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuongoza safari ya majaribio ya treni ya reli ya kisasa (SGR) itakayofanya safari kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma ikiwa na watu takriban 600. Majaribio hayo yatafanyika Aprili 21, 2024.  Katika treni hiyo Majaliwa ataambatana na viongozi wa Serikali, dini na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenda Dodoma…

Read More

Mbivu, mbichi suala la kikokotoo kujulikana Mei Mosi

Dodoma. Serikali imesema suala la kanuni mpya ya kikokotoo cha pensheni ya wastaafu lina maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan na limeanza kufanyiwa kazi, majibu yatajulikana kwenye sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi, jijini Arusha. Hayo yamesema leo Ijumaa Aprili 19, 2024 na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira…

Read More

Wafugaji Monduli walia bwawa kupasuka, kupoteza maji

Arusha. Wananchi wa jamii ya wafugaji katika kijiji cha Nanja kilichopo wilaya ya Monduli mkoani Arusha, wameiomba Serikali kuharakisha ukarabati wa kuta za bwawa la maji lililopo kijijini hapo, ambalo kuta zake zimevunjika na kusababisha maji mengi kupotea. Bwawa hilo la kuhifadhia maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kunyweshea mifugo, liliharibiwa na maji…

Read More

Mtoto adaiwa kujinyonga Arusha kisa kuchelewa shule

Arusha. Mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Olomitu iliyoko Chekereni jijini Arusha, Yusuph Zephania (13) anadaiwa kujinyonga hadi kufa kwa kuogopa adhabu itakayotolewa kwake baada ya kuchelewa shule. Tukio hilo limetokea jana April 18, 2024 nje ya nyumba katika kamba ya kuanikia nguo iliyokuwa nje. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP…

Read More

Hizi hapa dalili za changamoto ya afya ya akili kwa mjamzito

Mwanza. Kukosa usingizi wakati wa ujauzito, kujilaumu, kuwaza sana, kula sana na wakati mwingine kutokula kabisa ni miongoni mwa mambo yanayotajwa kuwa dalili za changamoto ya afya ya akili kwa mjamzito. Dalili hizo zimebainishwa leo Ijumaa Aprili 19, 2024 wakati wa kufunga mafunzo kuhusu changamoto ya afya ya akili kwa wajawazito na kina mama waliojifungua…

Read More

Dk Nchimbi awaonya wanaCCM udalali kwa wasaka uongozi

Njombe. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amewataka wanachama na viongozi wa chama hicho kujiepusha kuwa madalali wa watu wanaosaka nafasi za uongozi. Dk Nchimbi amesema kama kuna kitu kinachoweza kukidhoofisha chama hicho tawala ni viongozi kukubali kuwa madalali wa wagombea. “Mtu anayetaka kukufanya uwe dalali tafsiri yake ameshakupima, amegundua unanunulika,…

Read More

 Simbachawene amjibu Mpina | Mwananchi

Dodoma. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene amemshukia mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina akimtaka kutodharauliana. Simbachawene amesema hayo leo Aprili 19, 2024 alipojibu hoja za wabunge walizotoa walipochangia bajeti ya ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2024/25. Amesema nchi ambayo Mpina anasema imefeli inawezaje kutekeleza…

Read More