Nkwimba Hillu: Uthubutu ulimtoa darasani hadi kandarasi za mamilioni
Dar es Salaam. Alipoajiriwa kuwa mwalimu wa sekondari mwaka 2013 katika Shule ya Sekondari Mwatulole, mkoani Geita, aliamini ndoto yake ya kuajiriwa serikalini imeanza kutimia. Lakini siku aliyosaini mkataba na kuona mshahara wake wa ‘take home’ wa Sh470,000, moyo ulishtuka. Alijua fedha hiyo isingetosha kumudu maisha ya kupanga nyumba, kusaidia familia na kujikimu kwa mahitaji…