MJOMBA MATATANI KWA KUMPIGA NA KUMNING’INIZA MTOTO DIRISHAJI KWA KUUNGUZA MBOGA

 Jeshi la Polisi nchini Tanzania linamshikilia Joseph Mbalamwezi Francis Mkazi wa Mtaa wa Imalamakoe B, Wilayani Urambo, Mkoani Tabora kwa tuhuma za kumfanyia mtoto ukatili wa kufungwa kamba miguuni na mikononi na kisha kumning’iniza dirishani. Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania Naibu Kamishna wa Polisi DCP David Misime ameviambia Vyombo vya habari leo Jumatano  Machi…

Read More

Mtaalamu azungumzia faida, fursa katika sekta ya gesi

Dar es Salaam. Mtaalamu wa Nishati ya Gesi kutoka Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Mhandisi Geturu Bosinge, amesema watu wengi hawana ufahamu wa kutosha kuhusu faida za nishati ya gesi asilia katika matumizi mbalimbali, ikiwemo magari na mafuta. Amesema sekta ya gesi asilia ina fursa nyingi ambazo bado hazijafahamika wala kutumiwa kikamilifu na…

Read More

DG EWURA ASHIRIKI KIKAO CHA WADAU WAKUU WA MAFUTA NCHINI

********** Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Dkt James Mwainyekule, leo, 4 Machi, 2026 ameshiriki kikao cha ngazi ya juu cha wamiliki wa kampuni za bidhaa za mafuta aina ya petroli nchini (OMCs) kilichoitishwa na Waziri wa Nishati Mhe. Deogratias Ndejembi (Mb) ili kujadili mikakati ya iliyowekwa na serikali kuimarisha hali ya upatikanaji wa mafuta hususani kipindi…

Read More

Udhibiti dawa za kulevya Tanga wapunguza waraibu

Tanga. Upatikanaji wa dawa ya kulevya aina ya heroini umeelezwa kuwa mgumu katika Jiji la Tanga, hali inayotajwa kuwa matokeo ya kuimarika kwa udhibiti dhidi ya uingizwaji na usambazaji wa dawa hizo. Daktari wa afya ya akili katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo, Wallace Karata, amesema kupungua kwa upatikanaji wa heroini ni…

Read More

Wamachinga waliyoondolewa mitaa ya Uhuru na Msimbazi, Kariakoo

Dar es Salaam. Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imewaondoa wamachinga waliokuwa wakifanyabiashara katika barabara za Uhuru na Msimbazi, eneo la Kariakoo, katika utekelezaji wa tangazo lililotolewa awali kuwataka kuondoka katika maeneo yasiyoruhusiwa. Hatua hiyo ni utekelezaji wa tangazo lililotolewa na Mkurugenzi wa Jiji, Elihuruma Mabelya, Februari 17, 2026, lililobandikwa katika mitaa mbalimbali ya…

Read More

Sh7 bilioni zahitajika kudhibiti Mto Mbulumi wilayani Mvomero

Morogoro. Zaidi ya wananchi 1,200 wa vitongoji vya Msufini na Sokoni katika Kijiji cha Kichangani, Kata ya Mhonda wilayani Mvomero, wameiomba Serikali kuchukua hatua za haraka kudhibiti Mto Mbulumi uliobadili mkondo na kuingia katika makazi yao, hali iliyosababisha athari kwa zaidi ya kaya 700. Mafuriko yaliyotokea Februari 26, 2026 yamebomoa nyumba 20, huku nyingine zikiwa…

Read More

Bodaboda 3,000 wamepatiwa mafunzo udereva salama Mara

Musoma. Zaidi ya bodaboda 3,000 mkoani Mara wamepatiwa mafunzo ya udereva salama na sheria za usalama barabarani, katika mkakati wa Serikali mkoani humo kupunguza ajali zinazotokana na uendeshaji usiozingatia taratibu. Awali, bodaboda hao walikuwa wakifanya shughuli zao bila leseni wala mafunzo rasmi ya udereva, hali iliyochangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa ajali za barabarani. Hayao…

Read More

ENDELEENI KUIMARISHA UFUATILIAJI WA UTEKELEZAJI WA MTAALA ULIOBORESHWA.

Serikali imeitaka Taasisi ya Elimu Tanzania kuendelea kuimarisha ufuatiliaji wa tathimini ya utekelezaji wa  mitaala iliyoboreshwa ili kuleta matokeo chanya katika jamii. Hayo yamesemwa leo tarehe 4/3/2026 na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia  Mhe. Wanu Hafidh Ameir alipofanya ziara ya siku moja katika taasisi hiyo ili kupata uelewa wa majukumu mbalimbali yanayofanywa na…

Read More