Fundi wa boli Fountain gate ala kiapo

KIUNGO fundi wa mpira wa Fountain Gate, Elie Mokono aliyeisumbua ngome ya Simba jana usiku kwenye mechi ya Ligi Kuu Bara amekula kiapo akisema anaamini kikosi chao kitarejea katika mwenendo mzuri kama ilivyokuwa mwanzoni mwa  2024/25. Fountain Gate iliyolazimika kuivaa Simba ikiwa na wachezaji 13 na kupasuka kwa mabao 3-0 awali ilianza msimu kwa kuchapwa…

Read More

Saadun aona mwanga Azam FC

BAO alilofunga mechi ya kwanza ya Ligi Kuu dhidi ya Mbeya City limempa mzuka Nassor Saadun wa Azam aliyesema presha ya namba ndani ya kikosi imekuwa kubwa na kufunga kwake kumemuongezea morali. Saadun aliifungia timu hiyo ilipoibuka na ushindi wa mabao 2-0 jingine likifungwa na Feisal Salum ‘Fei Toto’ katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Azam…

Read More

Polisi yaanza kwa kipigo Zanzibar

UHAMIAJI imejiandikia rekodi ya kuwa timu ya kwanza katika Ligi Kuu Zanzibar kufunga bao na kupata ushindi ikiwa ugenini huku mchezaji wake akionyeshwa kadi nyekundu. Mechi iliyofanyika Septemba 25, 2025 kwenye Uwanja wa Mao A, Mjini Unguja, dakika 90 zilimalizika kwa Uhamiaji kutoka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi iliyopanda daraja msimu huu….

Read More

Simba, Yanga kuna kazi Oktoba 9

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetoa ratiba ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) itakayoanza kuchezwa kwa mechi za nusu fainali ya Ngao ya Jamii zitakazopigwa kwenye Uwanja wa KMC Complex, Mwenge Dar es Salaam. Timu zilizomaliza nafasi nne katika msimamo wa Ligi ya msimu uliopita ambazo ni bingwa mtetezi JKT Queens, Simba Queens,…

Read More

Ferry: Hatuna cha kupoteza kesho

Kocha wa Wiliete ya Angola, Bruno Ferry amesema timu yake haina cha kupoteza kwenye mchezo wa kesho ambapo  wataingia na akili ya kubadilisha matokeo. Ferry amesema wanatambua matokeo mabaya waliyoyapata nyumbani kwao ambayo yalitokana na uchanga wa kikosi  kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini wamejipanga kusahihisha makosa. “Baada ya mchezo wa kwanza tuligundua makosa yetu…

Read More

Yanga yashusha jezi mpya kuwakimbia ‘wafyatuaji’

Yanga imesema imeshusha mzigo wa jezi mpya awamu ya pili zitakazokuwa na mabadiliko ili kuwakimbia wahujumu wa mapato wanaofyatua jezi feki. Akizungumzia hilo, Meneja wa Habari wa Yanga, Ally Kamwe amesema mwekezaji wa biashara ya jezi za klabu baada ya kumalizika kwa jezi za kwanza ameshtukia uwepo wa uzi feki mwingi sokoni. Kamwe amesema baada…

Read More

Kamwe: Msipoona mafuriko kesho, nipigeni makofi

Msemaji wa Yanga, Ally Kamwe ametoa ahadi nzito kuelekea mchezo wa kesho wa Ligi ya Mabingwa Afrika, akisema kama Yanga isiposhinda kwa kishindo atakubali kupigwa makofi. Akizungumza klabuni hapo, Kamwe amewatoa wasiwasi mashabiki wa timu hiyo wenye wasiwasi na timu yao akisema mfumo uwanjani umeshakubali. Kamwe amesema wameshajaribu kila kitu kuelekea mchezo huo wa marudiano…

Read More

Folz kuwashushia mziki Waangola Kwa Mkapa

KOCHA wa Yanga, Romain Folz amesema kikosi kipo tayari kwa mchezo wa marudiano dhidi ya Wiliete akidai  atawashushia mziki kamili Waangola katika mchezo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika utakaopigwa Kwa Mkapa, kesho. Akizungumza leo, Folz amesema hana presha na lolote juu ya kikosi chake kwa kuwa kipo njia salama na kwamba…

Read More

Mashabiki Simba waibeba adhabu ya CAF

SIMBA inajiandaa kushuka uwanjani keshokutwa dhidi ya Gaborone United ya Botswana katika pambano la marudiano ya raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika bila mashabiki kutokana na adhabu iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF). Simba imeadhibiwa na CAF kutokana na matukio ya fujo zilizofanywa kwenye mechi za msimu uliopita za Kombe la Shirikisho…

Read More