Ukonga inavyozalisha mastaa wa kike Dar
KILE kituo cha Ukonga Basketball Academy ndicho kinachoongoza kwa ukuzaji wa vipaji vya wasichana katika Jiji la Dar es Salaam ambapo wengi wao wameonekana kutawala katika timu zinazoshiriki Ligi ya Kikapu mkoani humo (WBDL). Baadhi ya mastaa wa kike wanaotesa katika ligi hiyo ni pamoja na Monalisa Kaijage, Witness Mapunda, Ana Marie na Noela Uwendameno…