Rasmi mzigo umerudi | Mwanaspoti

ZIMEPITA siku 83 tangu kumalizika kwa msimu uliopita wa Ligi Kuu na leo mzigo umerudi upya ikiwa ni saa 24 baada ya kupigwa kwa mechi ya Ngao ya Jamii iliyozikutanisha Simba na Yanga. Msimu uliopita ligi ilifungwa na pambano la Dabi ya Kariakoo iliyopigwa Juni 25 na leo inaanza kwa mechi mbili zitakazopigwa jijini Dar…

Read More

Ligi Kuu 2025/26: Hizi zitapigwa sana na jua

RATIBA ya Ligi Kuu Bara 025-2026 imetoka ambapo pazia litafunguliwa kesho, Septemba 17, 2025 kwa KMC kuikaribisha Dodoma Jiji saa 10:00 jioni huku Coastal Union ikipambana na Tanzania Prisons saa 1:00 usiku. Mwanaspoti linakuletea timu zitakazokuwa na mechi nyingi saa 8:00 mchana zikiwemo Mashujaa, Tanzabia Prisons, KMC, Mbeya City, Pamba Jiji, Tabora United, Namungo na…

Read More

Yanga sasa wababe wa Kariakoo Dabi

Yanga imeendeleza ubabe kwa Simba baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa fainali ya Ngao ya Jamii uliochezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Shujaa wa Yanga katika mchezo huo alikuwa ni Pacome Zouzoua aliyefumania nyavu katika dakika ya 54 ya mchezo. Ushindi huo umekuwa ni wa sita mfululizo…

Read More

JKT Queens yanyakua ubingwa CECAFA

HATIMAYE JKT Queens imetawazwa kuwa bingwa wa michuano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) Wanawake baada ya kuitandika Rayon Sports ya Rwanda bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa leo Septemba 16, 2025 kwenye Uwanja wa Moi Kasarani jijini Nairobi nchini Kenya. Bao la Winifrida Gerald dakika ya tano akifunga kwa kichwa baada ya kumalizia…

Read More

Yanga wenyeji, Simba wageni watatu

YANGA imewaweka nje wachezaji wapya wote, ikianza na kikosi chenye wenyeji huku Simba ikija na wapya watatu. Yanga inacheza dhidi ya Simba kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii unaofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwenye kikosi cha Yanga kilichoanza, hakuna ambaye amesajiliwa dirisha kubwa lililofungwa Septemba 7 mwaka huu. …

Read More

Simba, Yanga zapishana dakika 12 kwa Mkapa

TIMU za Simba na Yanga tayari zipo ndani ya Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya mchezo wa Ngao ya Jamii utakaoanza saa 11:00 jioni. Yanga ndio imekuwa ya kwanza kufika hapa Benjamin Mkapa ikiwasili saa 9:22 alasiri, lakini ikashtua kidogo. Kilichofanyika, Yanga ikaibukia kusikojulikana ikitokea kwenye moja ya njia ya vumbi, kisha walinzi wake…

Read More

Kante, Pacome waibua presha Dabi ya Kariakoo

MUDA mchache kabla ya mchezo wa Ngao ya Jamii unaozikutanisha Yanga dhidi ya Simba, kuna presha iliibuka kwa mashabiki wa pande zote. Tukianza na Yanga, mashabiki wengi walianza kutishwa na taarifa kwamba kiungo wao fundi, Pacome Zouzoua hatakuwa sehemu ya mchezo huo. Hiyo ilitokana na Pacome kutoonekana kucheza mechi ya kilele cha Wiki wa Mwananchi…

Read More

Morogoro kuandika historia kwa Mkwawa Rally ya Afrika

Tanzania inajiandaa kuandika historia ya kuwa mwenyeji wa mbio za magari za ubingwa wa Afrika 2025, Mkwawa Rally of Tanzania, zitakazofanyika kuanzia Septemba 19 hadi 21 mkoani Morogoro. Zaidi ya madereva 23 kutoka mataifa mbalimbali wanatarajiwa kushiriki katika mashindano hayo yatakayohusisha jumla ya kilometa 338. Mashindano haya yanatarajiwa kuwa na ushindani mkali, hasa kati ya anayetabiriwa…

Read More

Metacha, Al Hilal wang’ara tuzo za CECAFA Kagame Cup

KIPA wa Singida Black Stars,  Metacha Mnata ameibuka kipa bora wa mashindano ya Kombe Kagame (Kagame Cup) yaliyofikia tamati jana Septemba 15, 2025 jijini Dar es Salaam. Mbali na Metacha, timu ya Al Hilal ya Sudan imetwaa tuzo ya ‘fair play’ katika mashindano hayo, tuzo waliyobidhiwa na mwakilishi kutoka Times FM, katika hafla ya utoaji…

Read More

Bado Watatu – 30 | Mwanaspoti

NIKAMJIBU: “RAISA, akijua, urafiki hautakuwepo tena kwa sababu nilimficha ukweli; na isitoshe, huyo Shefa alikuwa rafiki yake sana.”“Sasa msubiri baba yako aje umueleze; usikie atakwambia nini.”“Baba utamueleza wewe. Mimi siwezi kumueleza.”“Basi msubiri. Aliniambia anakwenda benki. Pengine muda huu anarudi.”Wakati mama ananiambia hivyo, Raisa akanipigia simu. Nikaipokea.“Habari ya huko, shoga?” akanisalimia.“Nzuri. Umeamkaje?”“Nashukuru, kumekucha. Ndiyo, nakufuata —…

Read More