Ni dhahir sasa, Gamondi haiwezi TRA United

KOCHA wa Singida Black Stars, Miguel Gamondi ni kama haiwezi TRA United (zamani Tabora United) baada ya jana jioni kuendeleza rekodi mbovu mbele ya Watoza Ushuru hao kwa kukubali kichapo cha mabao 3-1 kwenye Uwanja wa KMC Complex Mwenge jijini Dar es Salaam. Kama hujui TRA enzi ikiwa Tabor United ndio iliyompoza Gamondi akapoteza kibarua…

Read More

Siri ya Geita Gold ikisaka pointi 12

GEITA Gold inazidi kuchanja mbuga katika vita ya kupanda daraja kwenda Ligi Kuu msimu huu, huku ikiendelea kugawa vichapo kwa wapinzani na kutuma ujumbe kuwa imejipanga vyema kwa safari hiyo mpya. Timu hiyo inaongoza Ligi ya Championship ikiwa na alama 22 katika michezo minane ikiwa imeshinda saba na sare moja ikifunga mabao 18 na kuruhusu…

Read More

Sikia simulizi ya Bajaber simba

KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Mohamed Bajaber amesimulia namna alivyokuwa anapitia wakati mgumu kipindi alipokuwa anasumbuliwa na majeraha na ilibaki kidogo aondolewe kikosini bila kuonja mechi ya mashindano. Japokuwa Bajaber alikiri wachezaji wenzake walikuwa wanampa moyo, lakini hilo halikumuondolea kujisikia vibaya na kutamani itokee siku moja acheze mechi ya Ligi Kuu Bara kama alivyopata nafasi dhidi…

Read More

Beki Mtanzania anapambania namba Taifa Stars

BEKI raia wa Tanzania, Jackson Kasanzu anayekipiga Tormenta FC ya Marekani baada ya kuitwa kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha timu ya taifa ‘Taifa Stars’ kitakachowania Fainali ya Mataifa ya Afrika (AFCON), kwake ni jambo la fahari. Fainali hizo zitakazofanyika nchini Morocco kuanzia Desemba 21, 2025 hadi Januari 18, 2026, timu ya taifa ya…

Read More

TAFCA Mwanza yamkingia kifua Matola

CHAMA cha Makocha Tanzania (TAFCA) Mkoa wa Mwanza kimeungana na baadhi ya mashabiki na wadau wa soka nchini wanaompigia chapuo kocha mzawa Selemani Matola kuaminiwa na Simba na kupewa jukumu la kukinoa kikosi hicho moja kwa moja. Matola amedumu Simba kama kocha msaidizi kwa takriban miaka 10 akiwa chini ya makocha wengi wa kigeni katika…

Read More

SMZ yaahidi kuimarisha sekta ya michezo Zanzibar

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema  itaendelea kutoa ushirikiano katika kuhakikisha sekta ya michezo inaimarika zaidi na kutoa faida chanya kwa wanamichezo. Hayo yamesemwa leo Jumapili Desemba 7, 2025 na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla katika bonanza la mchezo wa mazoezi ya viungo, lililofanyika Kinduni, Kaskazini Unguja.  Hemed amesema, hayo…

Read More

Bao la Dube bado lamliza Kulandana

KIUNGO wa Fountain Gate, Abdallah Kulandana bado anaweweseka na kipigo cha mabao 2-0 ilichopewa timu hiyo na Yanga, huku akilitaja bao la Prince Dube lililotokana na penalti kuwa ndilo lililowatoa mchezoni na kujikuta wakipoteza mechi hiyo inayokuwa ya sita msimu huu. Kipigo hicho kilichopatikana kwenye Uwanja wa KMC kilikuwa cha pili mfululizo kwa timu hiyo…

Read More

Coastal v Yanga vita ipo hapa!

WAGOSI wa Kaya, Coastal Union usiku wa leo watakuwa wenyeji wa Yanga katika mechi ya Ligi Kuu Bara, huku wakiwa na rekodi ya unyonge wa kupasuka mechi nane mfululizo mbele ya watetezi hao tangu 2022, jambo lililowafanya mabosi wa klabu hiyo kushtuka na kuapa leo ni leo. Coastal inaipokea Yanga kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini…

Read More