Stars yalazimishwa sare ya kwanza CHAN

TIMU ya taifa ‘Taifa Stars’ imelazimishwa suluhu na Afrika ya Kati kwenye mechi ya mwisho ya kundi B iliyopigwa katika  Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam. Stars ilishafuzu mapema robo fainali baada ya kuichapa Madagascar mabao 2-1 siku chache zilizopita kwa mabao yaliyofungwa na Clement Mzize ambaye leo hakuwa sehemu ya mchezo. Stars ambayo iliingia…

Read More

Samatta, Le Havre waanza na kipigo

NYOTA wa kimataifa wa Tanzania na nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta ameanza vibaya Ligue 1 baada ya kikosi anachokitumikia kwa sasa Le Havre kulala kwa mabao 3-1 ikiwa ugenini mbele ya Monaco. Samatta aliyesajiliwa hivi karibuni aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Simon Ebonog dakika ya 58, lakini haikuisaidia kuepuka kipigo hicho kwenye…

Read More

Umemsikia Niyonzima Yanga? | Mwanaspoti

JANA, mashabiki wa Yanga waliwaona wachezaji wao wapya akiwemo akiwemo Balla Moussa Conte, Lassine Kouma, Mohamed Doumbia na mshambuliaji wa kati Andy Boyeli kwenye mechi hiyo ya kirafiki ambayo waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Rayon Sports mjini Kigali, Rwanda. Katika mechi hiyo iliyomalizika kwa Yanga kushinda 3-1, Rayon Sports ndio waliokuwa wa…

Read More

Camara aomba radhi mashabiki Guinea

MSHAMBULIAJI wa timu ya taifa ya Guinea, Ismael Camara amewaomba radhi mashabiki wa timu hiyo kufuatia sare ya kufungana bao 1-1 na Algeria iliyowaondoa kwenye nafasi ya kuwania kufuzu robo fainali ya Michuano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN). Guinea chini ya kocha Souleymane Kamara ilitangulia kupata bao kupitia kwa Camara dakika…

Read More

El Mami Tetah : Stars ilituumiza kichwa

MSHAMBULIAJI wa Mauritania, El Mami Tetah amefichua kwamba licha ya kupoteza mbele ya Taifa Stars katika mechi ya kundi B, mshikamano wa kikosi chao umewawezesha kumaliza makundi wakiwa na pointi saba. Mauritania ilipoteza mechi moja, ikitoa sare moja na kushinda mbili – matokeo ambayo yameifanya ishike nafasi ya pili kwenye msimamo kabla ya mechi za…

Read More

Kassali aibuka shujaa Niger ikitolewa CHAN 2024

KIPA wa timu ya taifa ya Niger, Mahamadou Kassali amesema walipaswa kushinda dhidi ya Afrika Kusini mechi ya Kundi C kwani walipata nafasi tatu za kufunga lakini walikosa kuzitumia. Mchezo huo uliopigwa Ijumaa kwenye Uwanja wa Nelson Mandela na kumalizika kwa sare tasa umeiondoa Niger kwenye mbio za kufuzu robo fainali baada ya kukusanya pointi…

Read More

Karia: Hatuendi kulipa kisasi | Mwanaspoti

Muda mfupi baada ya kuchaguliwa kwa kishindo kuendelea kuliongoza Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), rais Wallace Karia amesema hawana muda wa kulipa kisasi. Karia akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufunga mkutano wa uchaguzi huo ambao umefanyika katika Hoteli ya Tanga Resort mjini humo amesema licha ya uongozi wake kupitia nyakati ngumu, lakini hawatalipa…

Read More

Mahakama yakataa shauri la mwanahabari aliyeutaka urais TFF

Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam, leo, Jumamosi, Agosti 4, 2025 imekataa kusikiliza shauri lingine lililokuwa limefunguliwa dhidi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kuhusiana na uchaguzi wake mkuu. Uchaguzi Mkuu wa TFF umefanyika leo Jumamosi, Agosti 16, 2025, jijini Tanga, ambapo Wallace Karia amechaguliwa tena kuwa rais wa TFF kwa muhula…

Read More

CHAN 2024: Afrika Kusini yalia na VAR

TIMU ya taifa ya Afrika Kusini ‘Bafana Bafana’ imebidi kusubiri mechi za mwisho za kundi C baada kutoka suluhu dhidi ya Niger huku ikilalamikia VAR mara mbili. Huko Afrika Kusini kwa sasa mjadala ni namna ambavyo teknolojia hiyo ilivyowatibulia ushindi wa pili – matokeo ambayo yameifanya kuwa na pointi tano sawa wa Algeria inayoshika nafasi…

Read More