Freddy arudi ghafla, ajifua na mastaa wa Yanga

BAADA ya kusepa Simba, mshambuliaji Freddy Kouablan amerejea nchini kimya kimya, lakini akashtua kujifua na mastaa wa Yanga. Freddy ambaye alitua Simba dirisha dogo msimu uliopita akitokea Green Eagles ya Zambia akiwa amefunga mabao 11 yaliyomfanya awe Mfungaji Bora mwishoni mwa msimu wakati akiwa Msimbazi, aliondoka Simba hivi karibuni kumpisha Leonel Ateba kutoka USM Alger…

Read More

Walioing’oa Coastal kuvaana na Ninja CAF

BEKI wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga FC Lupopo ya DR Congo, Abdallah Shaibu ‘Ninja’ amefungukia fursa iliyopata timu anayoichezea kwa sasa kukutana na Bravos do Maquis raundi ya pili za Kombe la Shirikisho Afrika, huku akikiri haitakuwa mechi rahisi kutokana na ubora wa Waangola. Bravos ilipenya hatua hiyo baada ya kuvuka raundi ya kwanza kwa…

Read More

Nyota Prisons aonya makipa Bara

KIUNGO Mshambuliaji wa Tanzania Prisons, Zabona Hamis amesema dakika 180 bila timu kupata bao ni huzuni kwao, akieleza kuwa kurejea kwa pacha wake Samson Mbangula makipa wajipange. Prisons imeanza Ligi Kuu msimu wa 2024/25 kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana katika mechi mbili ilizocheza ugenini dhidi ya Pamba Jiji na Mashujaa na kushtua mashabiki…

Read More

Niyonzima, Coastal kuna jambo lipo

WIKI chache tangu aiachane na aliyekuwa kocha mkuu, David Ouma, klabu ya Coastal Union ya Tanga inadaiwa imemshusha kimyakimya kocha mpya kutoka Burundi, Domonique Niyonzima ambaye kwa sasa anaendelea kusimamia mazoezi yanayoendelea kambini eneo la Kigamboni, jijini Dar es Salaam. Licha ya kwamba mabosi wa Coastal bado haijatangaza rasmi juu ya kocha huyo ambaye ni…

Read More

Noela apoteza 90 za kwanza Ulaya

BEKI wa kati wa ASA Tel Aviv inayoshiriki Ligi ya Israel, Mtanzania Noela Luhala amepoteza mchezo wa kwanza akiwa na klabu mpya akitumika kwa dakika zote 90 dhidi ya KG Women Soccer kwa mabao 2-0. Mchezaji huyo wa zamani wa Yanga Princess inayoshiriki Ligi ya Wanawake nchini ni mara ya kwanza kucheza nje ya mipaka…

Read More

Samatta uso kwa uso na Manchester United

NYOTA wa kimataifa wa Tanzania na nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta mwezi huu anatajiwa kuanza kucheza mechi za michuano ya Ligi ya UEFA Europa League akiwa na klabu ya PAOK ya Ugiriki, huku akitarajiwa kuja kukutana uso kwa uso Man United, Novemba 7 mwaka huu. Katika droo ya michuano hiyo inayoendeshwa kwa mtindo wa…

Read More

Dakika 45 za Manula alivyorejea Simba

Jana Jumamosi, Aishi Salum Manula alirejea kwenye milingoti mitatu ya Simba tangu mara ya mwisho aonekane katika majukumu yake Machi 6 mwaka huu. Manula ambaye amekuwa nje ya kikosi cha Simba kwa takribani miezi mitano, alikuwa akiuguza majeraha ya nyonga, lakini baada ya kupona alichelewa kujiunga na wenzake baada ya kuwepo sintofahamu kutokana na nafasi…

Read More

Madina sasa awaita Wakenya, Waganda

Baada ya kushinda michuano mitatu mikubwa nchini Zambia na Uganda, Mtanzania Madina Iddi anawasubiri tena Wakenya na Waganda jiini Arusha ambako mashindano ya wazi ya gofu ya wanawake yatafanyika katikati ya mwezi huu. Yakijulikana kama Tanzania Ladies Open, haya ni mashindano ya gofu ya siku tatu ambayo yatapigwa katika mashimo 54  ya viwanja vya gofu…

Read More

Patwa, Khan waipaisha Mikumi | Mwanaspoti

MIKUMI imefanikiwa tena kuishinda Ngorongoro  katika mchezo wa pili wa majaribio kwa wachezaji nyota wa timu ya taifa ya kriketi uliopigwa jijini katika uwanja wa Anadil Burhan mwishoni mwa juma. Timu hizi ni kombaini zinazoundwa na wacjhezaji wa timu ya taifa kwa ajili ya kuwaandaa kwa michezo ya kufuzu fainali za kombe la dunia ambapo…

Read More