Mavambo aipa jeuri Simba SC

MSIMU uliopita, ungemwambia shabiki wa Simba kwamba mabosi wa klabu yake watamuacha kiungo wao Fabrice Ngoma wangeweza kukutia ngumi achilia mbali kung’aka kwa mshtuko. Lakini mechi mbili tu ndani ya msimu mpya ukiongeza na zile dakika 45 alizocheza katika Simba Day, zimetosha kumuibua mfalme mpya wa eneo la kiungo cha ulinzi, Debora Fernandes Mavambo. Huwaambii…

Read More

Aziz Ki amwachia Dube kiatu

WAKATI Yanga jana ilikuwa uwanjani kuvaana na Kagera Sugar katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara msimu huu iliyopigwa kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba, staa wa timu hiyo Stephane Aziz Ki ameamua kujisalimisha mapema kwa kumtaja mrithi wa kiatu cha Mfungaji Bora akimpa Prince Dube. Aziz Ki anayeichezea Yanga kwa msimu wa tatu,…

Read More

Kitasa cha Simba SC chatangaza vita mpya

BEKI wa kati wa Simba, Abdulrazack Hamza amesema, anajisikia vizuri ndani ya kikosi hicho tangu ajiunge nacho msimu huu akitokea SuperSport United ya Afrika Kusini, huku akiweka wazi hahofii ushindani wa namba uliopo na kwamba amekuja kupambana na sio kuuza sura Msimbazi. Nyota huyo aliyewahi kutamba na timu mbalimbali hapa nchini zikiwemo Mbeya City, KMC…

Read More

AKILI ZA KIJIWENI: Simba Queens imevuna ilichokipanda

MATUMAINI yalikuwa makubwa sana kwa Simba Queens kwamba ingetwaa ubingwa wa mashindano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) kwa wanawake yaliyofikia tamati jana huko Ethiopia. Mashindano hayo yako chini ya usimamizi wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) na bingwa wake hupata moja kwa moja tiketi ya…

Read More

Simba yawashtukia Al Ahli yatega mitego mitatu

SIMBA wajanja. Tayari viongozi wa timu hiyo wamekaa kikao na kuamua ni namna gani wataicheza mechi ya mkondo wa kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika ugenini Libya dhidi ya Al Ahli Tripoli na sasa wametega mitego mitatu wanayoamini ikifanikiwa basi wana uhakika wa kushinda ugenini jijini Tripoli. Simba na Tripoli zitakutana Septemba 13 mwaka huu…

Read More

Risasi, Veta nusu fainali Shinyanga

Timu ya Risasi imeinyoa B4 Mwadui kwa pointi 69-64 katika mchezo wa mwisho wa mzunguko wa pili wa  Ligi ya Kikapu Mkoa wa Shinyanga na kuifanya itinge nusu fainali ya ligi hiyo inayochezwakwenye Uwanja wa Mwadui, mkoani humo. Kwa matokeo hayo, Risasi iliongoza katika mzunguko huo kwa  pointi 11, ikifuatiwa na Kahama Sixers  iliyopata pointi…

Read More