NOELA: Chama wa Kikapu MVP mara 10

UKIMUONA nje ya kazi unaweza kumdharau, lakini ukija kazini kwake utapata stori ya namna anavyosifika kwa uchezaji uwanjani. Noela Uwandameno (22), ambaye ni mchezaji wa Vijana Queens na mwanafunzi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere anasimulia namna alivyoingia kwenye mpira wa kikapu na anavyojigawa pia kwenye masomo. “Ni miaka saba sasa tangu nianze kucheza…

Read More

Beki mpya JKT aota makubwa

BEKI mpya wa JKT Tanzania, Abdulrahim Seif Bausi aliyesajiliwa kutoka Uhamiaji ya Zanzibar, amesema anatambua Ligi Kuu Bara ni ngumu na inahitaji utulivu na kujituma, ili aweze kung’ara msimu ujao. Beki huyo ni mtoto wa kocha wa timu ya taifa ya Zanzibar ‘Zanzibar Heroes’, Seif Bausi, alisema alikuwa anaifuatilia ligi ya Bara, hivyo haoni kama…

Read More

Yanga yampa miwili beki Mkenya

YANGA inaendelea kushusha vyuma na safari hii imetua kwa beki wa kati raia wa Kenya, Anitha Adongo kwa ajili ya msimu ujao. Hadi sasa Yanga Princess inayoshiriki Ligi ya Wanawake (WPL) inahusishwa kumalizana na wachezaji wanne wa kigeni akiwemo Danai Bhobho kutoka kwa watani zao, Simba Queens. Akizungumza na Mwanaspoti, Rafiki wa karibu wa mchezaji…

Read More

MTU WA MPIRA: Simba msichonge sana, subirini kwanza ligi ianze

USAJILI wakati mwingine ni kama kamari. Unaweza kupatia. Pia unaweza kukosea. Ni ngumu kubetia usajili utakliki moja kwa moja. Hutokea mara chache sajili zikabamba. Ilitokea kwa Emmanuel Okwi alipotua Simba mara ya kwanza na hata alipokuwa akija na kuondoka. Lakini alichemka aliposajiliwa Yanga. Kuna Kipre Tchetche alipotua Azam. Usajili wake ulikuwa na maana kubwa. Azam…

Read More

Vital’O yapata pigo, Yanga ishindwe yenyewe

HII inaweza kuwa habari njema kwa Yanga baada ya wapinzani wao kwenye hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Vital’O kuzuiwa kutumia uwanja wao wa nyumbani wa Intwali uliopo Bujumbura, Burundi. Ukaguzi uliofanywa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (Caf) umebaini kuwa uwanja huo wa Intwali hauna sifa za kutumika kwa mashindano ya…

Read More

Yanga, Simba zapewa ubingwa Afrika

Dar es Salaam. Makocha na nyota wa zamani wa soka nchini wamezitabiria makubwa timu za Tanzania Bara zinazoshiriki mashindano ya klabu Afrika msimu ujao huku wakiamini zinaweza kutwaa ubingwa. Katika Ligi ya Mabingwa Afrika, Tanzania itawakilishwa na Yanga na Azam wakati kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, wawakilishi ni Simba na Coastal Union. Kwa mujibu wa…

Read More

Kina Diarra watishia kujiondoa Mali kisa sakata la Traore

Dar es Salaam. Kufuatia kusimamishwa kwa nahodha wa timu ya Taifa Mali, Hamari Traoré wachezaji wenzake wametishia kujiondoa kwa pamoja kwenye kikosi hicho kwa kile walichokitaja uonevu kwa nahodha wao. Nahodha huyo amefungiwa kwa kosa la yeye na baadhi ya wachezaji wenzake kumfokea na kumsonga mithili ya kumpiga mwamuzi Mohammed Adel raia wa Misri katika…

Read More

Tchakei kulamba dili jipya Singida

UONGOZI wa Singida Black Stars (zamani Ihefu), umeanza mazungumzo ya kumwongezea mkataba mpya kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Marouf Tchakei. Raia huyo wa Togo aliyejiunga na kikosi hicho Januari mwaka huu akitokea Singinda Fountain Gate aliyojiunga nayo kutokea AS Vita ya Congo, amekuwa na kiwango bora na msimu uliopita alifunga mabao tisa ya Ligi Kuu…

Read More