Sikia alichosema beki mpya Yanga, awataja Bacca, Azizi KI

WAKATI Yanga ikiwa katika hatua za mwisho za kukamilisha mazungumzo kwa ajili ya kumsajili beki wa FC Lupopo, Chadrack Boka anayetakiwa kuja kuziba nafasi ya Lomalisa Mutambala, mwenyewe amefunguka kwamba: “Najua mashabiki wanachotaka, waambie wasubiri nakuja kuwafurahisha kwa kuipa timu kazi nzuri.” Boka ambaye ni mrefu kwa umbo, amefichua kwamba anasubiri uhamisho huo ukamilike haraka…

Read More

Wydad yamganda Lakred, ishu nzima ipo hivi

TIMU ya Wydad Casablanca imeonyesha nia ya kumsajili kipa wa Simba, Ayoub Lakred kwa ajili ya msimu ujao. Taarifa kutoka ndani ya timu hiyo zimeliambia Mwanaspoti kwamba nyota huyo raia wa Morocco anataka kuondoka msimu ukiisha baada ya mkataba wake wa mwaka mmoja kumalizika jambo linalowatia wasiwasi mabosi wa Simba wanaomtaka abaki. Lakred aliyejiunga na…

Read More

Ouma anavyoibeba Coastal Union Ligi Kuu

KOCHA Mkuu wa Coastal Union, David Ouma amefanikiwa zaidi kutengeneza timu kimbinu na kiufundi, akijitahidi kumfanya kila mchezaji kuwa bora katika nafasi yake. Kocha huyo ambaye alianza kuifundisha Coastal Union, Novemba 9, mwaka jana akichukua mikoba ya Mwinyi Zahera ambaye alishindwa kuendana na kasi ya timu hiyo tayari ameanza kuandika rekodi zake ndani ya kikosi…

Read More

Dabo anazitaka 12 Azam FC

MATARAJIO ya Azam FC kwa sasa ni kukusanya pointi 12 katika mechi nne zilizosalia za Ligi Kuu Bara huku ikiiombea Simba iteleze kidogo tu ili wao wasiikose nafasi ya pili itakayowafanya washiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao. Hesabu hizo za Azam zinaonekana kuwa ngumu kidogo lakini wenyewe wana matumaini hayo licha ya…

Read More

Vita nane mpya ligi kuu

NDANI ya Ligi Kuu Bara achana na nani anataka kuwa bingwa, kuna vita fulani zinachukua nafasi taratibu nje na kuwania taji la ubingwa. Zitazame vita nane ambazo zinapatikana kivyake kwenye msimu huu wa ligi hiyo ukiwa unaelekea ukingoni ambazo zimekuwa zikizalisha ushindani mwingine. Simba kamchapa Azam juzi kwa mabao 3-0 ukiwa ni mchezo ambao ulikuwa…

Read More

Yanga yashtukia mtego, Gamondi aita kikao na mastaa

MASHABIKI wameshaanza kushona jezi za Ubingwa wa Yanga msimu huu, lakini Kocha Miguel Gamondi ameshtukia mechi mbili zinazofuata zina mtego mkubwa kwao na akawaweka chini wachezaji wake. Gamondi ameliambia Mwanaspoti amewasisitiza wachezaji wake wasijisahau kwani wanakwenda kucheza na timu ambazo zimechukua tahadhari kubwa kuliko kawaida na zina malengo mengi. Kocha huyo amesisitiza anaamini kila mchezaji…

Read More

Staa Asec aomba kusepa, atajwa kutua Simba

KIUNGO mshambuliaji wa Asec Mimosas, Serge Pokou ameomba rasmi kuondoka klabuni hapo huku akihusishwa na Simba inayoelezwa inampigia hesabu kali. Fundi huyo wa mguu wa kushoto ambaye aliwahi kuifunga Simba hapa nchini wakati timu hizo zilipokutana Ligi ya Mabingwa alisema ingawa ana ofa nyingi lakini amevutiwa na ofa ya Tanzania. “Nina ofa nyingi ikiwemo moja…

Read More

CITY BULLS, JKT PAMOTO DAR KESHO

UWANJA wa kikapu wa DB Osterbay unatarajiwa kuwaka moto wakati timu kongwe za kikapu nchini, JKT na Vijana (City Bulls) zitakapochuana kesho katika mchezo wa Ligi ya Kikapu ya Mkoa wa Dar es Salaam (BDL). Mchezo huo unasubiriwa kwa hamu na wapenzi wa kikapu mkoani humo kutokana na upinzani mkubwa zilio nao timu hizo.  Timu…

Read More

Thiago Silva kama kawa amemalizia hisani nyumbani

YUKO wapi yule aliyesema hisani inaanzia nyumbani? Wazungu huwa wanaandika kwa Kiingereza chao kizuri ‘charity begins at home’. Ni kweli. Lakini Wabrazil nao wangeweza kuendeleza sentensi hiyo na kuandika ‘hisani pia inaishia nyumbani’. Wiki ile nyingine nilimuona Mbrazili Thiago akilia katika viunga vya uwanja wa mazoezi wa Chelsea, Cobham. Labda ana hisia kali na Chelsea…

Read More