Manahodha Bara watia neno kanuni za Ligi Kuu

WAKATI kumekuwa na mijadala kuanzia mtaani hadi mitandaoni kuhusu kanuni za Ligi Kuu Bara msimu huu ambao zimeonekana kuuma kwelikweli, baadhi yaa mastaa na manahodha wa klabu za ligi hiyo wameshindwa kujizuia na kuzungumza. Kama hujui, kuna baadhi ya kanuni za Ligi Kuu zinazowahusu moja kwa moja wachezaji lengo likiwa ni kulinda nidhamu ya mechi…

Read More

Azam vs Yanga kupigwa Chamazi

MAJIBU ya maswali kuhusu wapi Dabi ya Dar es Salaam kati ya Azam FC dhidi ya Yanga katika Ligi Kuu itachezwa yamepatikana baada ya Uwanja wa Benjamin Mkapa kufungiwa kupisha maboresho yanayolenga Fainali za Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) 2027. Dabi hiyo itakayochezwa Machi 15, 2026 imehamishiwa Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es…

Read More

Hasheem Thabeet kuanza na haya kikapu

RAIS mpya wa TBF, Hasheem Thabeet amesema mambo mazuri yanakuja baada ya kuchaguliwa kuliongoza shirikisho hilo la mpira wa kikapu nchini akigusia ligi ya kikapu kupigwa mikoa yote. Thabeet ambaye ni mchezaji wa zamani wa Ligi ya Mpira wa Kikapu ya NBA alisema ligi ambayo ni maarufu nchini kwa sasa ni ya Dar Es Salaam…

Read More

Fountain Gate yailaza Mbeya City kwao

MBEYA City imeendelea kuwa na matokeo ya kusuasua kwenye Ligi Kuu Bara baada ya kuchapwa bao 1-0 na Fountain Gate kwenye mechi kali ya kufunga mzunguko wa kwanza kwa timu hizo iliyopigwa leo Machi 3, 2026 kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya. Mbeya City ambayo ipo chini ya kocha mzoefu, Mecky Maxime, haijafanya vizuri kwenye mechi…

Read More

Serikali kukamilisha maandalizi mkakati kukabiliana na wanyama wakali

Arusha. Serikali imesema inaendelea kukamilisha maandalizi ya Mkakati wa Kitaifa wa Kukabiliana na Wanyamapori Wakali na Waharibifu (2025/26–2034/35) pamoja na kufanya tafiti za kimkakati ili kubuni mbinu mpya za kukabiliana na wanyamapori hao, hususan tembo. Aidha, imeielekeza Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (Tawiri) kuendelea kuwafunga mikanda ya mawasiliano tembo viongozi ili kubaini mienendo yao…

Read More

Yanga Soccer School kuanza kusaka mastaa kitaa

YANGA inaendelea na mikakati ya kuhakikisha mpira wa miguu hapa nchini unakua na kutengeneza vijana waliopitia njia sahihi za kulelewa katika misingi inayotakiwa ili kuzitimiza ndoto zao. Hivi karibuni, klabu hiyo ilitangaza programu ya Yanga Soccer School, ambapo awamu hii umeongezeka udhamini wa GSM Foundation ili kuwasaidia vijana wasiokuwa na uwezo kifedha lakini wana vipaji…

Read More

Barker: Ile suluhu, tatizo Diarra

SIMBA imerejea nyumbani ikitokea Zanzibar ilikotoka sare dhidi ya mtani wake Yanga pale Uwanja wa Amaan Complex, Zanzibar huku kocha Steve Barker akiwasifia mastaa wa kikosi hicho na kumtaja kipa Djigui Diarra kwamba ndiye aliyezuia ushindi wa Wekundu hao. …

Read More

Kuelekea siku ya wanyamapori miti zaidi ya 2,700 yapandwa Arumeru

Arusha. Kuelekea maadhimisho ya siku ya Wanyamapori duniani yanayofanyika kila mwaka, Machi 3, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wameendelea na wiki maalum ya shughuli za uhifadhi wa mazingira, ikiwemo upandaji wa miti ya dawa na ya manukato. Maadhimisho hayo yanatarajiwa kufanyika Kitaifa kesho mkoani Arusha, yataongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Ashatu…

Read More

Mshambuliaji Mtanzania asimulia athari mgogoro Iran

WAKATI hali ya taharuki ikiendelea kuripotiwa katika baadhi ya maeneo ya Mashariki ya Kati kufuatia mshambulizi ya Israel na Marekani dhidi ya Iran, imeripotiwa wachezaji watatu wa Kitanzania wanaokipiga katika ukanda huo wako salama. Wachezaji hao ni mshambuliaji Simon Msuva anayekipiga Al Talaba ya Ligi Kuu Iraq, Clara Luvanga (Al Nassr, Saudia) na Morice Sichone…

Read More