Majitaka kero sugu Kariakoo | Mwananchi
Dar es Salaam. Haijalishi ni kipindi cha mvua au kiangazi, kero ya majitaka kutoka kwenye chemba za baadhi ya mitaa ya Kariakoo jijini Dar es Salaam imeendelea kuwatesa wafanyabiashara, mamalishe na maelfu ya watu wanaofika eneo hilo kwa shughuli za kibiashara. Katika mitaa kadhaa ikiwamo ya Uhuru, Msimbazi na Sikukuu, kumekuwa na majitaka yanayotiririka barabarani,…