Wizara ya Viwanda yataja mikakati 12, vijana watajwa

Dodoma. Kuelekea siku 100 za Rais Samia Suluhu Hassan madarakani tangu alipoapishwa kwa muhula wake wa pili, Wizara ya Viwanda na Biashara imetaja mambo 12 ambayo yamepewa mkazo mkubwa ikiangazia kundi la vijana. Katika kutekeleza mipango hiyo, mikopo 193 yenye thamani ya zaidi ya Sh820 milioni imetolewa na kuzalisha ajira 546, mingi ikiwagusa vijana.  Waziri…

Read More

Simba yaweka rekodi mpya ya vipigo CAF

WANASIMBA wanataka kuiona timu yao inafuzu robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kama kawaida yake ilivyofanya misimu saba iliyopita kuanzia 2018, lakini sasa mlima ni mrefu kutokana na matokeo iliyopata katika mechi tatu za kundi D. Kupoteza mechi tatu mfululizo za makundi katika michuano ya CAF, imekuwa ni matokeo mabaya zaidi kwa Simba kuyapata…

Read More

CCM Pwani: Malezi bora ni nguzo ya amani

Kibaha. Wazazi mkoani Pwani wametakiwa kuimarisha malezi kwa vijana ili kuwajengea misingi ya amani, nidhamu na uzalendo, huku wakihimizwa kuepuka vitendo vya vurugu vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa nchi. Wito huo umetolewa leo Jumamosi, Januari 24, 2026, na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hamoud Abuu Jumaa, wakati wa…

Read More

Kamati ya Bunge: Vijana wawezeshwe mitaji, zana za kazi

Dodoma. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imeitaka Serikali kuweka mifumo madhubuti ya kuwawezesha wahitimu wa vyuo vya ufundi stadi kupata mitaji na zana za kazi. Kamati hiyo imebainisha kuwa vijana wengi hushindwa kutumia na kuendeleza ujuzi walioupata mara baada ya kuhitimu kutokana na ukosefu wa rasilimali hizo. Imesisitiza kuwa uwezeshaji…

Read More

Kiongozi wa CWT Morogoro afariki dunia kwa ajali

Morogoro. Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Morogoro kimepata pigo kufuatia kifo cha mwenyekiti wake, Mbaruku Ligubi (46), aliyefariki dunia baada ya kupata ajali ya barabarani iliyotokea usiku wa Januari 22, 2026. Mwalimu Ligubi aligongwa na gari katika ajali iliyotokea saa 2 usiku katika barabara kuu ya Dar es Salaam – Morogoro, eneo la…

Read More

Sh249 milioni kuboresha zahanati ya shule ya mahitaji maalumu

Rungwe. Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya imetumia zaidi ya Sh249 milioni kuboresha miundombinu ya zahanati katika Shule ya Msingi Katumba II Mchanganyiko. Shule hiyo inayohudumia wanafunzi wenye mahitaji maalumu, imepewa fedha hizo kuweka mazingira wezeshi ya upatikanaji wa huduma bora za afya kwa kundi hilo. Hatua hiyo imeelezwa kuwa mwarobaini wa changamoto za…

Read More