Simba yaweka rekodi mpya ya vipigo CAF
WANASIMBA wanataka kuiona timu yao inafuzu robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kama kawaida yake ilivyofanya misimu saba iliyopita kuanzia 2018, lakini sasa mlima ni mrefu kutokana na matokeo iliyopata katika mechi tatu za kundi D. Kupoteza mechi tatu mfululizo za makundi katika michuano ya CAF, imekuwa ni matokeo mabaya zaidi kwa Simba kuyapata…