Ujenzi daraja la Kigongo – Busisi kukamilika Aprili 30
Mwanza. Serikali imesema ujenzi wa daraja la Magufuli (Kigongo – Busisi) utakamilika rasmi Aprili 30, 2025 na kuanza kutumika rasmi. Hata hivyo, hadi kufikia Aprili 10, 2025, magari yataanza kupita upande mmoja wa barabara kwenye daraja hilo lenye urefu wa kilomita tatu ambalo ujenzi wake kwa sasa umefikia asilimia 97. Daraja hilo linaunganisha barabara kuu…