Beki Simba haonekani kambini | Mwanaspoti

WAKATI sakata la mshambuliaji wa Simba Queens, Aisha Mnunka likiwa bado halijaisha, limejibuka jipya kuhusu beki wa timu hiyo Mkongomani Daniella Ngoyi ambaye naye haonekani klabuni na hajatoa taarifa. Daniella anakuwa mchezaji wa pili kuondoka kambini bila taarifa baada ya awali Aisha ambaye tangu Simba Queens itangaze hawamuoni, bado hajatokea kikosini hapo. Simba Queens ipo…

Read More

Yanga ni Mokwena au Mfaransa

MABOSI wa Yanga, wameendelea kufanya yao kimyakimya katika mchakato wa kusaka kocha atakayepewa nafasi ya kuiongoza timu hiyo kwa msimu ujao huku zoezi hilo likichukua sura mpya baada ya kuamua kuliongeza jina la kocha mmoja kutoka nyumba ya vipaji raia wa Ufaransa. Yanga ipo katika mipango ya kutemana na Miloud Hamdi anayeionoa kwa sasa ambaye…

Read More

Djuma Shaban atimkia Ufaransa | Mwanaspoti

BEKI wa zamani wa Yanga, Djuma Shaban anayekipiga Namungo kwa sasa, ametimka nchini kwenda Ufaransa, huku akifunguka kilichofanya aende huko akiwa amepewa muda wa wiki moja kabla ya kurejea kikosini kuungana na wenzake kujiandaa na mechi za Ligi Kuu Bara. Djuma aliyewahi kuitumikia AS Vita ya DR Congo kabla ya kutua Yanga misimu mitatu iliyopita,…

Read More

Mnoga amaliza kibabe chama jipya la Beckham

BEKI wa Kitanzania, Haji Mnoga anayekipiga Salford City ya England amemaliza kibabe msimu akifunga bao moja na asisti nne. Huu ni msimu wa kwanza kwa beki huyo wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ kuitumikia timu hiyo akitokea Aldershot aliyeichezea kwa misimu miwili. Mnoga alicheza mechi 39 kati ya 46 za timu hiyo kwa dakika 3306…

Read More