Hiki hapa chanzo cha ahaji ajali migodini

Dar es Salaam. Wakati mara kadhaa Serikali ikinyooshewa kidole pale zinapotokea ajali kwenye migodi, Kamishna Msaidizi Wizara ya Madini, Terrence Ngolo amesema ajali hizo haziwezi kuisha kutokana na watu kukiuka maelekezo ya wataalamu. Amesema wakati mwingine ajali hizo hutokea kwa uzembe hasa pale wachimbaji wanapokiuka maelekezo ya tahadhari yanayotolewa na wataalamu. Ngolo amesema hayo leo…

Read More

Saa moja ya Zuchu jukwaani kwa Mkapa

Takriban saa nzima ya Zuhura Othuman maarufu Zuchu katika tamasha la Wiki ya Mwananchi imetosha kutoa burudani ya aina yake kabla ya mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya Yanga na Bandari FC. Zuchu ametumia majukwaa manne tofauti akiimba nyimbo zake zaidi ya sita, huku akimrudisha jukwaani kwa mara ya pili D Voice kuimba naye…

Read More

NRA kuunda Serikali yenye Wizara 10 ikishinda uchaguzi

Mirerani. Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA), Almas Kisabya amesema endapo atachaguliwa kuwa Rais, ataunda Serikali ndogo yenye wizara zisizozidi 10, lengo likiwa kufanikisha utendaji kazi. Kisabya ameyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni ya urais leo Ijumaa Septemba 12 mwaka 2025 mjini Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara. Amesema endapo atachaguliwa…

Read More

Dk Biteko: Hakuna matokeo bila tathmini

Mwanza. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko amezitaka taasisi za umma na binafsi kuhakikisha zinafanya ufuatiliaji na tathmini ya mara kwa mara ili kujiandaa na athari zinazoweza kujitokeza, kwa kuwa tayari zitakuwa na suluhu mkononi. Amesema mtu au taasisi isiyofanya tathmini hujikuta ikishangazwa na matokeo badala ya kuyatabiri na kujiandaa mapema….

Read More

Majaliwa: Tutasaka kura Kitanda kwa kitanda

Nachingwea. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kitasaka kura kwa namna yoyote ile hata kama ni nyumba kwa nyumba, kitanda kwa kitanda shuka kwa shuka katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Akizindua kampeni katika Wilaya ya Nachingwea leo Ijumaa Septemba 12,2025 Majaliwa amesema kuwa wanaCCM wanatakiwa kusaka kura za Rais,…

Read More

Pacome wa mwisho akifungwa kamba na Manara

NI zamu ya Pacome Zouzoua kufungwa kamba ya viatu na Haji Manara katika utambulisho wa wachezaji msimu huu wa 2025/26 unaotarajia kuanza Septemba 17 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Msimu uliopita Manara alifanya hivyo kwa Stephane Aziz Ki, na pia aliwahi kufanya hivyo kwa Feisal Salum ‘Fei Toto’ wakati huo akiwa Yanga…

Read More