Kijana mbaroni kwa tuhuma za mauaji, uporaji wa pikipiki na fedha
Mbeya. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mawazo Msangawale (24), mkazi wa Mlowo mkoani Songwe, kwa tuhuma za kumuua kijana Juveni Baraka (18), kwa kumkata na kitu chenye ncha kali kichwani. Mbali na kutekeleza mauaji hayo, alifanikiwa kutoweka na pikipiki aliyokuwa akitumia marehemu na Sh1.5 milioni alizokuwa nazo marehemu kwa ajili ya kununua madini…