Mamlaka za ardhi zatajwa kuchochea migogoro Tanga
Tanga. Migogoro ya ardhi inayohusisha umiliki wa viwanja na urasimishaji wa makazi imekuwa changamoto kubwa kwa wakazi wa Jiji la Tanga, wakilalamikia taratibu za utoaji wa hati na usimamizi wa ardhi unaofanywa na halmashauri. Malalamiko hayo yameibuliwa katika Kliniki ya Sheria ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliyoweka kambi ya siku saba mkoani Tanga,…