Mahakama kutoa uamuzi kesi ya bosi wa Jatu, Machi 14
Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepanga Machi 14, 2025 kutoa uamuzi wa ama kumuondolea mashitaka na kumfutia kesi Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Jatu PLC, Peter Gasaya(33) au kuendelea na kesi hiyo. Uamuzi huo umetolewa leo, Machi 11, 2025 na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Geofrey Mhini baada ya kusikiliza hoja za upande wa mashitaka…