Mukwala asepa, aibukia Uarabuni | Mwanaspoti

KAMA Mwanaspoti lilivyowajulisha mapema baada ya Jean Charles Ahoua kuuzwa CR Belouizdad ya Algeria, pia Steven Mukwala naye alikuwa mbioni kuondoka klabuni hapo, ndivyo ilivyo kwa sasa baada ya straika huyo raia wa Uganda kutua Al-Nasr ya Libya. Licha ya Mukwala jana  kucheza mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar na Simba ilibanwa…

Read More

Sh300 milioni kuimarisha kilimo cha mwani Zanzibar

Unguja. Katika kuendeleza na kuimarisha kilimo cha mwani Zanzibar, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar wamezindua mradi wa utafiti wa zao hilo na matumizi ya teknolojia kuchochea ukuaji wake. Mradi huo unaotarajia kutumia Sh300 milioni, mbali na Zanzibar utafanyika pia Mafia na Bagamoyo kwa…

Read More

Mkurugenzi Mkuu TAA aondolewa kesi ya mgogoro wa ardhi KIA

Arusha. Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Moshi, imeruhusu kuendelea kwa kesi ya ardhi inayohusu mgogoro wa ardhi baina ya baadhi ya vijiji vinavyopakana na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Aidha, Mahakama hiyo imetupilia mbali sehemu ya pingamizi la awali lililowasilishwa na wadaiwa likipinga uhalali wa kesi hiyo, kwa madai kuwa wadai waliwashtaki…

Read More

Kigongosi: Viongozi wa halmashauri msiwe chanzo cha migogoro

Singida. Viongozi wa halmashauri nchini wameonywa kutokuwa chanzo cha migogoro ya wao kwa wao na badala yake watambue kazi yao ni kuwatumikia wananchi kwa nafasi zao bila kuwabagua. Mbali na viongozi wa halmashauri, wasimamizi wa miradi wametakiwa kutanguliza utu kwa wafanyakazi ikiwemo kutowadhulumu stahiki zao na walipe kwa wakati kile walichokubaliana. Wito huo umetolewa leo…

Read More

Gofu yakusanya Sh112 milioni za kutibu macho

MASHINDANO Maalumu ya Gofu ya Dar es Salaam Mzizima ‘Lions play for Sight’ yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Gymkhana yakishirikisha wachezaji 70, yamekusanya jumla ya Sh112 milioni, zitakazotumika katika kuchangia huduma ya macho. Mratibu wa mashindano hayo, Ragib Hassanali amesema wachezaji hao wanatoka klabu za gofu za Lugalo, Morogoro Gymkhana  na Dar es Salaam Gymkhana na…

Read More

Magata atambia rekodi mpya Mtibwa Sugar

KIUNGO mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Fredrick Magata amesema kufunga bao katika mechi ya Ligi Kuu Bara akiwa na kikosi hicho msimu huu kwake ni rekodi mpya katika maisha yake, kwani hajawahi kufanya hivyo, tangu ameanza kucheza maishani. Nyota huyo aliifungia Mtibwa Sugar bao la kusawazisha dakika ya 60, katika mechi ya Ligi Kuu dhidi ya…

Read More

Wanaodaiwa kusafirisha heroini, waendelea kusoka rumande

Dar es Salaam. Upelelezi kesi ya kusafirisha dawa za kulevya inayowakabili Abdallah Mwita (38)  na wenzake watatu haujakamilika. Wakili wa Serikali, Roida Mwakamele ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo, Januari 19, 2026 wakati kesi hiyo ilipotajwa. Mwita na wenzake wanakabiliwa  na kesi ya uhujumu uchumi namba 5208 ya mwaka 2025, yenye mashtaka mawili ya…

Read More