Wanaodaiwa kutakatisha Sh346 milioni za CRDB, NBC wamwangukia DPP
Dar es Salaam. Raia wa Bulgaria, Eduardl Mladenov (32) na Mtanzania Juma Ndambile (58) wanaodaiwa kujihusisha na miamala ya kutoa fedha katika Benki za CRDB na NBC, wamemuandikia barua Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), wakiomba kufanya majadiliano ya kukiri makosa (plea bargaining) ili kuimaliza kesi inayowakabili. Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka sita, yakiwamo ya kuongoza genge…